Gazeti la Tanzania Daima la tarehe 23 Januari, 2013 liliandika makala inayosomeka "JK
AMNUSURU MFUNGWA WA ERA". Gazeti hilo lilidai mfungwa wa kesi ya
ERA Ajay Somani ametolewa gerezani kwa njia ya kutatanisha wakati wafungwa
wengine waliokuwa kesi moja wanaendelea kusota gerezani.
Maelezo mafupi kuhusu suala hilo ni kwamba mfungwa Na. 74/2012 Ajay
Suryakant Somani tarehe 22 Novemba, 2012 alihukumiwa kifungo cha miaka miwili
na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu shauri la Jinai Na. 1164/2008 kwa kosa la "Obtaining
Money by False Pretence c/s 302 of the Penal Code".
Watuhumiwa wenzake katika kesi hiyo walikuwa Sophia Joseph Lalika, Ester
Komu na Emmanuel Mwakyosa. Hawa walikuwa wanakabiliwa na shtaka la "Occasioning
Loss to a Specified Authority". Hawa walihukumiwa
kifungo cha miaka mitatu au faini shilling! milioni tano (Tzs.5,000,000/=) kila
mmoja. Wafungwa wawili Ester Komu na Emmanuel Mwakyosa walilipa faini siku hiyo
hiyo mahakamani na kuachiliwa huru. Mfungwa Sophia Joseph Lalika kwa kuwa hakulipa
faini hiyo mahakamani alipelekwa gerezani na tarehe 23/11/2012 alilipa faini
hiyo na kuachiliwa huru. Hivyo madai yaliyotolewa kwamba bado wanasota
gerezani siyo ya kweli.
Kuhusu Mfungwa Na. 74/2012 Ajay Suryakant Somani wakati akiendelea na
kifungo chake gerezani alipata mapunguzo ya 1/6 ya kifungo chake kwa msamaha wa
Rais uliotolewa kwa wafungwa tarehe 9 Desemba, 2013 wakati wa kuadhimisha
miaka 52 ya Uhuru wa nchi yetu. Mapunguzo haya ya 1/6 ni zaidi ya
mapunguzo ya kawaida 1/3 yanayotolewa chini ya Sheria ya Magereza ya mwaka 1967.
Kutokana na msamaha huo kifungo chake kupunguzwa kwa nusu (1/3
+ 1/6 = 1/2) yaani mwaka mmoja na kwa hali hiyo kustahili
kuachiliwa huru tarehe 9/12/2013.
Wafungwa
wengine waliotajwa No.247/2011 Farijala Shabani anayetumikia kifungo cha
miaka kumi na moja (11) na Na. 345/2011 Rajabu Maranda anayetumikia kifungo
cha miaka kumi (10) nao walinufaika na msamaha huo wa Mhe. Rais lakini
waliendelea kubaki gerezani kutokana na urefu wa vifungo vyao.
Hivyo Gazeti husika lifute kauli hiyo kwa kuwa waliachiliwa huru kwa
mujibu wa sheria na kwa sasa ni raia huru.
John C.
Minja
KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA
23 Januari, 2014
Nafikiri makosa ya wizi wa mali ya umma hasiwe na msamaha!!
ReplyDeleteKwa nini Tz inachukulia makosa ya EPA kama makosa ya kawaida.? Mbona huu NI UHUJUMU UCHUMI.Nadhani,si mbali ,itabidi turevew makesi mengi kama haya,na tuongeze watuhumiwa.Wanajijua,wajitayarishe aisee!
ReplyDeleteasanteni Tanzania daima, Keep up informing us. Kamata kamata ya EPA na hukumu zake zilikuwa ni mchezo wa kuigiza. Fisadi kaiba TZS 10 billion, anafungwa kifungo cha miaka 11 bila ya kutakiwa kuzirudisha pesa hizo alizoiba. Akitoka kifungoni nakuwa huru kuzifukua pesa hizo na kula bata kilaini bila kudaiwa tena. Mbaya zaidi baada ya miaka 2-3 anapata msamaha wa raisi. Hii itaongeza wananchi kukosa imani na vyombo vya dola. AlexBura dar
ReplyDeleteVyombo vyetu vya habari havina umakini kabisa. This is a serious national challenge! Hawa ndio tunawatarajia kuutaarifu umma? Hivi walishindwa kumpigia msemaji wa Idara husika?
ReplyDeleteWandugu,
ReplyDeleteKulingana na Mchezo wa ulaji unavyo kuwa ni kwamba hiyo hela anakuwa mara zingine haja fanya Hujuma kwa gemu moja.
Anakuwa anakula muda baada ya muda huku akishirikiana na wengine!,,,kama ujuavyo ktk laji lazima wengine watachomoka na wengine kuliwa kafara hivyo atakaye liwa kafara ndiye atakaye pigiwa hesabu yooote ya hasara na kukuta Mabilini ya Shilingi, sioyo ktk Gemu moja inakuwa kwa muda mrefu wizi unafanyika.
Mkitaka muamini hicho kitu ni huyo mama mmoja Sophia Lalika yeye hakuwa na kitu hapo (Shs. 5 Millioni za Faini) ikabidi aende Lupango na ndipo ndugu zake nje wajikusanye ili Bi Mkubwa atoke Mukenge!!!