Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mwamuzi Methusela Msebula kilichotokea juzi (Januari 13 mwaka huu) katika Wilaya ya Bukombe mkoani Geita.

Mwamuzi Msebula ambaye alikuwa mwamuzi daraja la kwanza (class one) alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari, maradhi ambayo yalimsababisha kuwa nje ya uchezeshaji mechi za mpira wa miguu kwa karibu misimu miwili.

Msiba huu ni mkubwa kwa jamii ya mpira wa miguu kwani, Msebula alitoa mchango mkubwa katika fani ya uamuzi nchini, hivyo mchango wake tutaukumbuka daima. Marehemu anatarajiwa kuzikwa leo (Januari 15 mwaka huu) nyumbani kwao Kanyigo, Bukoba mkoani Kagera.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Msebula, Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu Tanzania (FRAT) na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Geita (GEREFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...