Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousfi (kulia) akinyanyua kwa furaha zawadi ya kinyago ambayo ni moja ya zawadi alizokabidhiwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto).Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe Youcef Yousfi ikiwa ni pamoja na ujumbe wake wamewasili nchini Tanzania. Nia na madhumuni ya ziara hiyo ni kudumisha ushirikiano katika sekta za nishati na gesi.
Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousfi (kushoto) akibadilishana mawazo na Waziri wa Nishati na Madini (kulia) Profesa Sospeter Muhongo mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousfi akichangia mada kwenye kikao hicho
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia ) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Aliyekaa upande wa kushoto ni Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria Mhe. Youcef Yousfi
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akizungumza na wakuu wa mashirika na idara wa Wizara ya Nishati na Madini ikiwa ni pamoja na ujumbe wa Waziri wa Nishati na Migodi wa Algeria uliowakilishwa na wakuu wa taasisi na mashirika
Baadhi ya wajumbe kutoka Wizara ya Nishati na Migodi ya Algeria wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa na wakuu wa Idara kutoka Wizara ya Nishati na Madini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...