Baadhi ya watoto yatima wa kituo cha Sifa Group Children Foundation Center kilichopo Bunju, Dar es Salaam wakiwapokea kwa furaha wafanyakazi wa Idara ya mauzo na Usambazaji wa kampuni ya Vodacom Tanzania wakati walipoenda kutoa msaada kwenye kituo hicho. Msaada huo wa chakula na vitu mbali mbali kupitia kampeni ya pamoja na Vodacom.
Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania kutoka kushoto ni Happiness Macha na Elihuruma Ngoi wakisaidia kushusha msaada wa chakula iliyotolewa na wafanyakazi wa Idara ya Mauzo na Usambazaji wa kampuni hiyo kwa kituo cha kulea watoto yatima cha Sifa Group Children Foundation Center kilichopo Bunju, Dar es Salaam kupitia kampeni ya Pamoja na Vodacom.
Mkurugenzi wa kituo cha kulea watoto yatima cha Sifa Group Children Foundation Center Bi. Sifa John kutoka kulia akipokea kiroba cha chakula kama sehemu ya msaada kupitia kampeni ya Pamoja na Vodacom, anaekabidhi (Katikati) ni Mkuu wa idara ya Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Julius Kastabu, (kushoto) ni Meneja wa Mipango na Uuzaji Baraka Bitebu.
BOFYA HAPA KWA HABARI ZAIDI
BOFYA HAPA KWA HABARI ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...