Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Z. Kabwe pamoja na Mwanasheria wake,Albert Msando (kulia) wakiwasili katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam leo huku wakiongozana na wafuasi wanaopinga kuvuliwa uongozi wake,tayari kwa kwenda kusikiliza kesi yake aliyoifungua dhidi ya Chama Chake cha CHADEMA inayosikilizwa leo Mahakama Kuu.
Mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini  ameshinda kesi yake hiyo aliyoifungua akiitaka Kamati Kuu ya Chadema kutojadili Uanachama wake hadi kesi ya msingi aliyoifungua itakaposikilizwa.
Habari zaidi utaendelea kuzipata hapa
Wafuasi wa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe wakimshangilia kiongozi wao alipokuwa akiwasili Mahakamani hapo leo.
Sehemu ya Wafuasi wa CHADEMA wasiomkubali Zitto Kabwe wakiwa na Mabango yao nje ya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam leo.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. THIS IS A VERY SAD PICTURE. MUNGU IBARIKI TANZANIA. Kwa kutumia maagizo ya mwalimu wangu wa lugha wa darasa la sita, ichunguze picha hii kisha uandike insha.

    ReplyDelete
  2. sasa hapa inshu ni kuwa CHADEMA hawataki kupeleka kesi ya ZZK kwenye Baraza Kuu ama? Maana huu mchezo wote wa redio unazidi kukiumiza chama. Mpelekeni tu Baraza Kuu msiogope kushindwa ndio demokrasia hio!!

    ReplyDelete
  3. Hao wafuasi na mabango yao wanaisadia au kuibomoa CDM? Au wanaonyesha tu true face ya chama chao!

    ReplyDelete
  4. Chadema ndembendembe..nyarinyari...chaliii pwaaaataaaa.

    ReplyDelete
  5. hayo matusi ndio demokrasia ya chadema? kuanzia uongozi wa juu mpaka wafuasi wake wote hekima hawana, busara ya mtu inaonekana kwa mazungumzo, muonekano, hata hayo mabango mliyobeba yangewaonyesha hekima zenu. hebu kaeni chini mtafakari, mtasema ni zito mbaya kumbe nyie wenyewe ndio wabaya:
    1. yawezekana mna ubinafsi katika uongozi wenu, hamshirikishani katika maamuzi.

    2.acheni uroho wa madaraka, la sivyo mwakani hampati kitu, bado siku tu uchaguzi. mnagombana wenyewe kwa wenyewe.

    3. slaa waachie wengine sasa uone nao watafanya nini?

    4. slaa nenda kwenu katengeneze chama kuanzia nyumbani kwako, maana kwako sidhani kama unakubalika, ukitengeneza kwako, kwingine itakuwa mteremko tu.

    4. mbowe, uache kauli kali, watanzania hawakuzoea hayo, ndiyo maana mnaona watoto ndio wengi kwenye mikutano yenu, mwisho wa kupiga kura hakuna kitu. rekebisheni kauli. waswahili husema kauli ni mali.

    5. ikiwa mtajirekebisha kwa hayo, hata mimi nitawapigia kura.

    michuzi usinibanie.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...