Mwenyekiti mpya wa TAHA, Bw. Eric Ng'imaryo, akizungumza mara baada ya kuchaguliwa kushika wadhifa huo. 
  Na Mwandishi Wetu TAASISI inayoshughulika na kilimo cha maua na mboga mboga nchini (Tanzania Horticultural Association -TAHA) imemteua Bw. Eric Ng'imaryo kama Mwenyekiti wake mpya kuchukua nafasi iliyoaachwa wazi na Bw. Colman Ngalo, ambaye ameiendesha taasisi hiyo kwa mafanikio kwa takribani miaka kumi ya utawala wake. Sambamba na uteuzi huo pia Bw. Ng'imaryo.
Pia taasisi hiyo imepata Makamu Mwenyekiti mpya pamoja na wajumbe wanane wa Bodi ya TAHA pia walichaguliwa katika Mkutano Mkuu uliofanyika hivi karibuni jijini Arusha.
 Miongoni mwa wanaounda Bodi mpya ya taasisi ya TAHA ni pamoja na: Bi. Fatma Riyami, Bw. Ravi Bhalerao, Bw. Herald Peeters , Bw. Juma Lossini, Bw. Robert Daniel, Bw. Tjerk Scheltema na Bw. Adrian Moss. 
Bw. Eric kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Bodi mpya ya TAHA na ni mategemeo yangu kuwa tutaendelea kufanya kazi pamoja naye katika miaka ijayo. Mchanganyiko wa ujuzi wake katika sekta ya maua na mboga mboga na uzoefu mkubwa sambamba na utaalamu unafanya kuwa mtu bora kuchukua nafasi ya Uenyekiti wa TAHA na sekta yenye maendeleo endelevu.
 "Napenda pia kuishukuru Sekretarieti ya TAHA na wanachama wake kwa ushirikiano wao bora katika muongo uliopita. Kwa ushirikiano tumepata mafanikio mkubwa. Mimi ninajisikia fahari kubwa kukabidhi taasisi hii yenye mafanikio ambayo bado ina fursa kubwa kwa ukuaji zaidi katika TAHA na sekta nzima kwa ujumla." 
 TAHA ni taasisi ambayo ni mwanachama wa sekta binafsi ambapo imekuwa ikishiriki kwa ufanisi katika kubadilisha kilimo cha sekta ya maua na mboga mboga toka kuanzishwa kwake mwaka 2004. 
 Kutokana wa hatua za uwepo wa TAHA , sekta ya maua na mboga mboga nchini na kufanikiwa kuvutia washirika mbali mbali kutoa misaada mikubwa ikiwa ni pamoja na serikali ya Tanzania na Washirika kama vile USAID, BEST- AC, Ubalozi wa Uholanzi , ITC, na Serikali Finland. TAHA inatoa sapoti mbali mbali kwa wadau wa sekta ya maua na mboga mboga ikiwemo kuwajengea uwezo kwenye majukwaa, kulinda na kukuza maslahi ya watendaji katika sekta hiyo ya maua yaani wazalishaji, wauzaji, wasindikaji, na watoa huduma ya maua, matunda , mboga, viungo, mimea na mbegu za maua

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...