Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi akizungumza na viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara katika siku ya pili ya kongamano la viongozi hao kuhusiana na rasilimali zetu za gesi asilia, mafuta na madinikwa amani na maendeleo ya Tanzania. Kongamano ambalo lilifanyika leo katika ukumbi wa VETA, Mtwara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) Yona Killagani akitoa mada juu ya Mipango ya Matumizi ya gesi asilia Lindi na Mtwara katika siku ya pili ya semina ya siku mbli ambapo leo ndio kilele cha kongamano hilo lililowahusisha viongozi wa dini katika mikoa hiyo.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Stella Maris Mtwara Padre Dkt. Aidan Msafiri akitoa mada ya Tunu na maadili katika rasilimali za gesi, mafuta na madini leo katika ukumbi wa VETA Mtwara kwa viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara ambapo alisisitiza kuwa mwanadamu amepewa jukumu la kuwa meneja wa rasilimali ikiwemo gesi. Kongamano ambalo lilifanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa VETA, Mtwara na kuwashikisha viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara.
Baadhi ya wanakongamano wakimsikliza Padre Dkt. Aidan Msafiri katika siku ya pili ya kongamano la viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara juu ya matumizi bora ya tunu za kimaadili, kiroho, akili, utashi, imani, haki na elimu adilifu ambapo mwanadamu amepewa jukumu la kuwa meneja wa rasilimali vitu ikiwemo gesi asilia, mafuta na madini.
Makam wa Askofu wa Kanisa la Kanisa la Anglikana Tanzania na Askofu wa Dayosisi ya Newalaa Oscar Mnung’a (wa kwanza kushoto) akifuatilia kongamano la viongozi wa dini kutoka mikoa ya Lindi na Mtwara lililofanyika katika ukumbi wa VETA Mtwara. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia.
BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI KAMILI
BOFYA HAPA KWA PICHA NA HABARI KAMILI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...