Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Bw. Abas Kandoro akifungua kongano la Muungano kwa vyuo vya elimu ya juu mjini mbeya leo, kushoto ni Naibu katibu Mkuu Ofisi ya makamu wa Rais Bi Angelina madete,na Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya muungano kutoka Ofisi ya makmau wa Rais Baraka Rajab
Waziri wa Nchi Ofisi Ya Makamo wa Rais Muungano Mh. Samia Suluhu Hassan akifafanunua kuhusu masuala ya Muungano katika kongamano lililohusisha vyuo vya elimu ya juu mkoani Mbeya leo.
Washiriki wa Kongamano la Muungano mkoani Mbeya ambao ni wanafunzi wa vyuo ya elimu ya juu wakifuatilia mjadala katika kongamano hilo mjini Mbeya leo.

Ni wajibu wa kila Mtanzania kutambua kwamba uandikishwaji wa katiba mpya unalenga kuweka misingi ya kuijenga Tanzania ya sasa naya siku nyingi zijazo.

Hayo yameelezwa leo na mkuu wa mkoa wa Mbeya Bwana Abas Kandoro katika ufunguzi wa kongamano la vyuo vya elimu ya juu mkoani humo,lililohusu masuala mbali mbali ya muungano kuelekea maadhimisho ya miaka hamsini ya muungano wa iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar.

Katika Kongamano hilo Bwana Kandoro aliongeza kwa kusema kuwa jambo hili ni kubwa na linahitaji umakini wa hali ya juu saana katika kila hatua ili kufanikisha mchakato huu, aidha Bwana kandoro aliwakumbusha washiriki wa kongamano hilo kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar umekuwepo kutokana na sababu nyingi lakini kubwa ni kuwepo kwa mahusiano ya karibu kihistoria baina ya Tanganyika na Zanzibar katika Nyanja mbali mbali kama vile undugu wa damu, biashara,utamaduni lugha na mahusiano ya karibu ya kisiasa.

Bwana kandoro aliendelea kusema kuwa, Muundo wa muungano wetu umeweka mfumo wenye vyombo mbalimbali vyenye mamlaka za utendaji, kutunga sheria na kusimamia shughuli za umma na utoaji haki.

“Pamoja na hiyo mifumo, na kuwepo sababu nyingi nzuri na za msingi za kuwepo Muungano, bado ndani ya jamii yetu kuna wanaohoji uhalali wake kupitia maoni yaliyotolewa mbele ya tume ya mabadiliko ya katiba mahakama na mijadala mingine, alisisitiza.”

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa yawezekana kabisa kuwa washiriki wanaweza kuwa na hoja zinazofanana na hizo..na hivyo mada zitakazotolewa zinaweza kusaidia kujibu baadhi ya hoja.

Katika Kongamano hilo wasomi hao wametoka na kauli mbiu inayosema “MUUNGANO IMARA NI MUSTAKABALI WA TAIFA LETU.”

Kungamano hili linaondeshwa na Idara ya Muungano ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika Mikoa ya Mbeya ya Iringa ni moja ya makongamano katika vyuo vikuu nchini kuelekea maadhisho ya miaka hamsini ya Muungano

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...