Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kupalilia katika shamba la Magreth Kalimwa (wapili kulia), katika Kijiji cha Mlimanyoka, Kata ya Nsalanga, wilala ya Mbeya mjini. Kinana alifika kumsaidia mkulima huyo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 37 ya CCM, inayofanyika Kitaifa Jumapili hii mjini Mbeya.

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na Bi.Magreth Kalimwa mara baada ya kuwasili kwenye shamba lake kwa ajili ya kushiriki kupalilia shamba hilo lenye ekari moja na nusu
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi na Wanachama wa CCM,(hawapo pichani) katika kijiji cha Itesi Mashariki,Kata ya Nshalanga,alipokwenda kukagua ujenzi wa jengo la Ofisi ya kata ya chama cha CCM,Wilaya ya Mbeya Mjini mkoani Mbeya mapema leo.
Ujenzi wa jengo la Ofisi ya kata ya chama cha CCM,Wilaya ya Mbeya Mjini mkoani Mbeya mapema leo kama ionekanavyo mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipokwenda kufanya ukaguzi
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akisaidiana na vijana kuandaa jukwaa litakalotumika wakati wa mapokezi ya matembezi ya maadhimisho ya miaka 37 ya CCM, kwenye Uwanja wa Sokine mjini Mbeya. Matembezi hayo yanaongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete
Vijana wakiwa kwenye mazoezi ya maadhimisho ya miaka 37 ya CCM yatakayofanyika Jumapili hii mjini Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...