Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa Sokoine ,ambapo alisema maandalizi yote yamekamilika ,majukwaa yamekamilika, uwanja umerekebishwa vizuri na vijana wa Halaiki wamejiandaa vya kutosha tayari kwa sherehe ya kuzaliwa kwa CCM tarehe 2 Februari.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akishiriki hatua za mwisho za maandalizi ya mahala ambapo maandamano yatahitimishwa.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na vijana wa Halaiki ambao watashiriki kuonyesha Halaiki kwenye kilele cha miaka 37 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi ambayo kitaifa yatafanyika mkoani Mbeya tarehe 2 Februari.
Jukwaa litakalotumika kwa burudani likiwa kwenye hatua za mwisho kufungwa kwenye uwanja wa Sokoine ambapo Band ya TOT na wasanii wa vizazi vipya wanategemewa kutumbuiza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. jamani naomba kuliza ccm ilizaliwa tar.2 au tar 5 mwezzi 2 77 sababu hii tar ilikua ya azimio la arusha ikawa tamasha la vijana mpaka ccm sasa naona hapa ina sema tar. 2 feb sielewi naomba mnikumbushe. maadhimisho mema

    ReplyDelete
  2. Vijana wa "halaiki".....watakaoshiriki kuonyesha "halaiki".....Wadau naomba kufahamishwa maana hasa ya neno hilo "halaiki" na kama ni sahihi kulitumia katika sentensi hizi kwenye hii habari.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...