Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya mawasiliano ya Airtel Tanzania Ijumaa hii itachezesha droo kubwa ya promosheni yake ya 'Mimi Ni Bingwa' ambayo itamfanya mmoja wa wateja wake kujishindia zawadi ya kitita cha shilingi milioni 50.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jane Matinde alisema droo hiyo itakayobadilisha maisha ya mtu, imepangwa kuchezeshwa katika ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.
"Baada ya miezi kadhaa iliyojaa zawadi kwa wateja wetu waaminifu, Ijumaa hii itakuwa ndiyo kilele cha promosheni yetu ya Mimi Ni Bingwa ambapo tutamtafuta na kumtangaza mshindi wa zawadi yetu kubwa," alisema.
Jane alisema kuwa mshindi atakayebahatika atapatikana kwa kuchezesha droo ya bahati na sibu utakaokuwa chini ya uangalizi na usimamizi wa afisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania na kushuhudiwa na wafanyakazi wa Airtel na vyombo vya habari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...