Mshambuliaji machachari wa timu ya Yanga,Mrisho Ngassa (17) akichuana vikali kuwania mpira na Beki wa Timu ya Mbeya City,Deogratias Julius wakati wa mtanange wa Ligi kuu Tanzania Bara uliomalizika hivi sasa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Dakika 90 za mchezo zimemalizika hivi punde na Yanga imeshinda kwa Bao 1-0 lililotiwa kimiani na Mrisho Ngassa,dakika ya 15 ya mchezo kipindi cha kwanza.
 Beki wa Timu ya Mbeya City,Deogratias Julius akijiandaa kuondosha hatari iliyokuwa imekwenda langoni kwao.

Kiungo mshambuliaji wa Yanga,Haroun Niyonzima  pamoja na Beki wa Mbeya City,Yussuf Abdallah wakiwania mpira,wakati wa mchezo wao wa marudiano katika mzungunguko wa pili wa Ligi kuu Tanzania Bara uliomalizika hivi sasa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Mashabiki wa Mbeya City wakiendelea kuishangilia timu yao.
 Mbuyu Twite wa Yanga akiangalia nani na kumpatia pasi wakati wa mtanange wa Ligi kuu Tanzania Bara uliomalizika hivi sasa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
 Wachezaji wa Yanga wakishangilia bao lao la kwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Msikate tamaa MBeya city, bao moja si kitu sana. Yanga ni timu ya muda mrefu sana kuliko ninyi. Hata hivyo mmejitahidi sana. Hongereni kaza mwendo.

    ReplyDelete
  2. Kwa waamuzi hawa wa kibongo kazi ipo.

    ReplyDelete
  3. Hatimaye Yanga yavunja mwiko wa Mbeya City!

    Hii ni Tambiko ya CCM kumimiza miaka 37 tena Maadhimisho yakifanyika hukohuko mjini kwenu Wanyampala wa Mbeya City!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...