TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 01.02. 2014.


MWANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI AFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA BARABARANI.

gari ambalo halikuweza kufahamika namba zake za usajili wala jina la dereva wake lilimgonga mtembea kwa miguu mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi mbuyuni aliyetambulika kwa jina la daima faida (08) mkazi wa mbuyuni na kusababisha kifo chake papo hapo. ajali hiyo ilitokea majira ya saa 06:55hrs asubuhi wilayani mbarali mkoa wa mbeya. chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi, dereva alikimbia mara baada ya tukio. mwili wa marehemu umekabidhiwa ndugu kwa ajili ya mazishi. juhudi za kumtafuta mtuhumiwa zinaendelea. kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi ahmed z. msangi anatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za mahali alipo mtuhumiwa wa tukio hili azitoe katika mamlaka husika ili akamatwe na sheria ichukue mkondo wake.


Signed by:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...