ABIRIA mmoja kati ya 28 amekufa papo hapo na wengine kulazwa Hospitali ya mkoa wa Lindi, Sokine,kufuatia basi la kampuni ya CHALA Express walilokuwa wakisafiria kutoka Jijini Dar es salaam kwenda wilaya ya Newala mkoani Mtwara, kukwaruzana na Lori.

Abiria aliyepoteza maisha katika ajali hiyo anaitwa Amina Omari Makodora (48) mkazi wa kijiji cha Kilindoni,wilaya ya Mafia,mkoani Pwani.

Kwa mujibu wa abiria wengine walionusulika kwenye ajali hiyo,wameiambia Globu ya Jamii kuwa ajali hiyo imetokea eneo la kijiji cha Kilangara,kilichopo katika Halmashauri ya wilaya ya Lindi,saa 8:0 mchana.

Abiria hao waliokuwa wakisafiri na basi hilo la kampuni ya Chala Express namba T. 699 ATK linaloendeshwa na dereva,Haji Chande Chondo (56) mkazi wa Jijini dar es salaam,linalofanya safari zake kati ya Jiji na Newala.

Dereva Chondo ameliambia gazeti hili Hospitalini hapo kuwa, wakati akiwa katika eneo hilo aliweza kukutana na Lori lililokuwa limebeba kijiko kutoka mikoa ya kusini na kuelekea wilayani Kilwa.

"Hili Lori lilikuwa linatelemka mlimani na mimi pia,hivyo mwenzangu akaniwashia taa na kunifanya nipunguze mwendo na kubana zaidi kushoto"Alisema Chondo.

Chondo alieleza kuwa wakati akiwa amejaribu kubana pembeni zaidi ndipo Lori hilo ambalo bado namba zake hazijaweza kufahamika mara moja, likamkwaruza sehemu ya ubavu wa kulia wa basi na kusababisha kifo cha mmoja wa Abiria wake na wengine kuumia sehemu mbalimbali ya miili yao.

Alisema mara baada ya kumkwaruza Lori hilo halikuweza hata kusimama badala yake aliendelea na safari yake bila kujali nini kimetokea au usalama wao.

Hatibu Nassoro mmoja wa abiria wa basi hilo, amesema kama gari yao ingekuwa katika mwendo mkali,lingeweza kupinduka na kusababisha maafa makubwa.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,Dkt, Muhaji Mohamedi amekili kupokea mwili wa marehemu Amina Omari Makodora,wakiwemo na majeruhi tisa (9) waliokuwa wakisafiri na basi hilo,huku mmoja akiwa bado hajaweza kutambuliwa mara moja.

Amewataja majeuhi hao kuwa ni,Asha Mohamedi Buriani (43),Zuhura Maulidi (28) mwenyeji wa Tandahimba,aliyeumia kichwani,Hadija Chiwaya (36),Asha Mohamedi (43) haji Chondo (56) ambaye pia ni dereva wa basi hilo.

Wengine ni Rashid Mchowanje (60) aliyeumia bega la mkono wa kulia na Anifa Mwenye (17) mwanafunzi wa kidato cha tatu Shule ya Sekondari Kiregezi kata ya Mkunya,wilaya ya Newala aliyepata michubuko mkono wa kulia na mwingine ambaye jina lake bado halijaweza kufahamika mara moja.

Dkt Muhaji amesema majeruhi watatu kati ya hao wamelazwa Hospitali wakiendelea na matibabu ambapo wengine sita wametibiwa na kuruhusiwa kuendelea na safari zao.

Kaimu kamanda wa Polisi mkoani Lindi,Joseph Mfungomara amekili kutokea kwa ajaili hiyo, na kueleza kuwa basi hilo lilikuwa na abiria 28,na kwamba Jeshi hilo linaendelea kumsaka dereva wa Loli aliyesababisha ajali na mauwaji wa abiria huyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...