KWA NIABA YA FAMILIA YA MZEE JOHN ALLONGA WA BUTURI RORYA, NAPENDA KUWAJULISHA NDUGU JAMAA NA MARAFIKI WOTE KUWA BIBI YETU MPENDWA MAGDALENA ONGUKA(MEME) AMEAGA DUNIA TAREHE 5.2.2014 KATIKA KIJIJI CHA BUTURI AKIWA NA UMRI WA MIAKA 108 MIPANGO YA MAZISHI YANAFANYIKA KIJIJINI BUTURI, BIBI AMEACHA WATOTO WANNE, WAJUKUU 35 NA VITUKUU 42.

TUTAPEANA TAARIFA YA TARATIBU ZITAKAVYOKUWA

Michael G.Allonga
Mjukuu wa Marehemu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Du! Mungu ampumzishe pema. Amefanya alichoagiza Mungu kwa binadamu hapa dunia. Watoto wanne na wajukuu 35!

    ReplyDelete
  2. Wewe mdau wa kwanza washangaa nini? Au hauishi Tanzania?? Kwa kijijini hao watoto wanne kuzaa watoto kama ifuatavyo unaona haiwezekani: 9 + 9 + 9 + 8??

    Au ukijumlisha hapo, haupati 35??

    ReplyDelete
  3. Masha Allah, angali anaonekana bado alikuwa na nguvu zake hapo pichani, Mwenyeez Mungu kamjaaliya uzao si haba, kadhalika na umri pia alijaaliwa wa kutosha si haba, kapumzike kwa amani Bibi yetu, MOLA akusamehe kwa yote na kukupumzisha palipo pema peponi - AMEN.

    Poleni sana ndugu, jamaa na marafiki wote wa marehemu Bibi Magdalena Onguka Allonga. Mwenyeez Mungu awape nguvu, faraja na stahamala katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na Bibi yetu mpendwa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...