Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam
Tanzania
inatarajiwa kuwa, miongoni mwa nchi 150 zitakazoshiriki maonesho ya 53 ya
Kimataifa ya madini ya vito na usonara yatakayofanyika Bangkok Thailand, kuanzia
tarehe 25 februari hadi tarehe 1 Machi, 2014.
Kutokana
na kuwa na hazina kubwa ya madini ya aina mbalimbali, Tanzania imealikwa kuwa
miongoni mwa nchi zitakazo shiriki maonesho hayo yanayojulikana kama ‘Bangkok
Gems and Jewelry Fair’.
Akizungumzia
ushiriki wa Tanzania katika maonesho hayo jana, Kamishna wa Madini, Mhandisi Paul Masanja alieleza
kuwa, Tanzania inatarajia kuyatumia
maonesho hayo kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Thailand katika biashara
ya vito na usonara, kutangaza madini ya vito yanayopatikana hapa nchini,
kutafuta masoko mapya ya biashara na bei za uhakika katika tasnia ya madini ya
vito, kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya kusimamia na kukabiliana na
changamoto zilizopo katika tasnia ya madini ya vito na usonara hapa nchini
ikiwemo pia kukubaliana maeneo ya kushirikiana.
Aidha,
aliongeza kwamba, maonesho hayo yatasaidia Tanzania kujifunza uzoefu wa kuandaa
maonesho ya Kimataifa ya vito na usonara ili kuboresha maonesho ya ‘Arusha
Internal Gem, Jewelry and Minerals Fair’ (AIGJMF) yanayofanyika nchini kila
mwaka.
Mkurugenzi
wa idara inayoshughulikia kuthamini Almas na madini mengine ya Vito, ‘Tanzania
Diamonds and Gemstones Valuation Unit’, (TANSORT) Bw. Archard Kalugendo, ameongeza
kuwa, ushiriki wa Tanzania vilevile unalenga kuwavutia wanunuzi na wauzaji
kununua bidhaa hizo moja kwa moja nchini badala ya manunuzi kufanyika katika nchi
na miji mengine mathalan Tanzanite ambayo kwa sasa inanunuliwa kutoka Hongkong,
Mumbai na Afrika Kusini, na madini ya Almas
kutoka India, Dubai na Antwerp.
Aliongeza
kuwa, ushiriki huo, utaiwezesha Tanzania kupata nafasi ya kutangaza fursa
mbalimbali za uwekezaji hususan katika madini ya vito yanayopatikana hapa
nchini, kutoa taarifa za tafiti mbalimbali, ugunduzi mpya na kuelezea mipango
endelevu iliyopo katika sekta hiyo.
Aidha,
mbali na ushiriki wa Wizara, Tanzania itawakilishwa na Shirika la Madini Tanzania (STAMICO), Kampuni
sita za wafanyabiashara wa madini za Isle of Gems, Suju Gem Ltd, Tom Gems, H.B
Mining Ltd, Swala Gems Traders, Gems and Rock Ventures. Aidha, kutakuwa na
uwakilishi wa shirikisho la wachimbaji Tanzania (FEMATA), (TAMIDA) na kampuni nyingine
za madini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...