Wakati zikiwa zimesalia siku zisizozidi elfu moja kufikia kikomo cha utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya milenia mwaka 2015 mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa mjini Geneva balozi Modest Jonathan Mero amesema sekta ya afya inahitaji msukumo zaidi katika kutekeleza malengo hayo.
Katika mahojiano maalum na idhaa hii Balozi Mero ambaye hivi karibuni alikutana na Mkuu wa shirika la afya duniani Magreth Chan, amesema anatarajia kukutana pia na mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la mapambano dhidi ya ukimwi UNAIDS katika juhudi za kujadili mbinu za kutekeleza lengo hilo la sita. Na hapa anaanza kwa kufafanua lengo la mkutano wake na mkuu wa WHO
(SAUTI MAHOJIANO)
Kusikiliza bofya hapa
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...