Mshindi wa promosheni ya Timka na bodaboda Bw. Ramadhani Abdallah akipiga kiki pikipiki yake tayari kuondoka nayo mara baada ya kukabidhiwa na Meneja Uhusiano wa Nje Salum Mwalim(kulia) katika tukio lililofanyika Mlimani City jijini Dar es salaam.

 Meneja  uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim akiongea na washindi wa promosheni ya Timka na bodaboda iliyomalizka hivi karibuni wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika Makako Mkauu ya Vodacom eneo la Mlimani City jijini Dar es Salaam.Jumla ya washindi 48 walikabidhiwa bodaboda zao zikiwa tayari zimeshasajiliwa.  
 Sehemu ya pikipiki zikiwa tayari kutolewa kwa washindi wa promosheni ya Vodacom ya Timka na bodaboda iliyomalizika hivi punde. Pikipiki hizo zilikabidhiwa kwa washindi katika hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Vodacom yaliyopo Mlimani City jijini Dar es salaam
 Sehemu ya pikipiki 48 zikiteremshwa kwenye viunga vya Makao Makuu ya Kampuni ya Vodacom tayari kwa ajili ya zoezi la kukabidhiwa kwa washindi wa iliyokuwa promosheni ya timka na bodaboda iliyomalizika hivi karibuni na kuhusisha wateja wa Vodacom
 Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Salum Mwalim (wa kwanza kulia) akifuatilia zoezi la kuhakiki taarifa za washindi wa bodaboda wa iliyokuwa promosheni ya timka na bodaboda iliyomalizika hivi karibuni. (Kutoka kushoto) ni Ofisa Uhakiki wa Viwango wa Vodacom Ombeni Urasa, Regan Rugangira (mshindi) na Ofisa Masoko wa Vodacom Prestin Lyatonga. Jumla ya washindi 48 walikabidhiwa bodaboda zao kwenye hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Vodacom, Mlimani City jijini Dar es salaam.
Mshindi wa promosheni ya Timka na bodaboda Bw. Japhet Shedrack akiondoa pikipiki yake mara baada ya kuhakikiwa na (Kutoka kushoto) Ofisa Uhakiki wa Viwango wa Vodacom Ombeni Urasa, Ofisa Masoko wa Vodacom Prestin Lyatonga, Salum Mwalim Meneja wa Uhusiano wa Nje. Jumla ya washindi 48 walikabidhiwa bodaboda zao kwenye hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya Vodacom, Mlimani City jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...