DSCF2699Kaimu kamishna Mkuu wa wa Mamlaka ya mapato Tanzania Rished Bade akizungumza na vyombo vya habari jijini Arusha kuhusu mgomo wa wafanyabiashara hapa Nchini
DSCF2695Waandishi wa habari wakiwa kazini
DSCF2697Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa walipa kodi Richard Kayombo
DSCF2713Mr.Jangala ambaye ni Ajenti wa usafirishaji wa magari ya mikoani akilalamikia hali ya wafanyabiashara kugoma ambapo anadai kuwa imemuathiri kwa kiasi kikubwa kukosa abiria wanaokuja kununua bidhaa za jumla
DSCF2700
DSCF2706Shughuli mbalimbali zilidorora hata zile za M-pesa
DSCF2711Hapa maduka yakiwa yamefungwa kama inavyoonekana katika picha eneo la maduka ya stendi mabasi yaendayo Moshi
DSCF2712
DSCF2708Muonekano katika stendi kubwa ya mabasi baada ya mgomo wa wafanyabiashara

Na Pamela Mollel,Arusha
Wafanyabiashara hapa nchi wametakiwa kutoendeleza mgomo  wa mashine za kieletroniki za EFD’S na badala yake wafungue maduka na kuendelea na biashara zao kwa kutumia mashine  kwa kufanya hivyo watakuwa wametimiza masharti ya kufanyabiashara.

Rai hiyo aliitoa jana Kaimu kamishna mkuu wa Mamlaka ya mapato Tanzania Rished Bade wakati akizungumza na vyombo vya habari jijini Arusha ambapo alisema kuwa kitendo cha kutumia mashine kwa wafanyabiashara itawawezesha kuweka  kumbukumbu sahihi.

Alisema kuwa kodi ya ongezeko la dhamani ilikuwa kwenye awamu ya kwanza hivyo  awamu ya pili wafanyabiashara hawatahusika kulipa kodi kama wengine wanavyodai
“siyo kweli kwamba wakitumia mashine watafilisika bali watakuwa na kumbukumbu sahihi…na kuna watu wachache wanapotosha wafanyabiashara kwa hili” alisema Bade.

Aidha aliwataka wafanyabiashara kutokubali kutumika na wasiowafanyabiashara ambao wamekuwa  wakiwashawishi kufunga maduka ili kushinikiza serikali bali wawaripoti katika mamlaka husika ili sheria ichukue mkondo wake

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. HAPA SWALA LA MSINGI NI BEI KUBWA YA MASHINE IKIWA PAMOJA NA GHARAMA ZA UENDESHAJI WA HIZO MASHINE. LAKINI KUBWA ZAIDI NI KWANINI UKIFUNGA BIASHARA HAUWEZI KIIUZA KWA MTU MWINGINE?

    ReplyDelete
  2. Aah wapi! Gharama za mashine hizo zimepunguzwa kutoka 1.2m mpaka 600,000/- Isitoshe, kama mfanya biashara angechukua accounting and inventory package, computer/laptop, learning curve, maintenance, internet access etc, wangekuwa wanalipa zaidi ya hizo EFD ambazo kwa laki 6 zinafanya inventory, stock taking, financials zingine, all these a big advantage katika kutunza kumbukumbu za mfanyabiashara anaye tumia hizi!!

    Somewhere somehow someone is being lied to big time!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...