Uchaguzi wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) utafanyika Machi 2, 2014 jijini Dar es Salaam.
Fomu kwa ajili ya waombaji uongozi zinaanza kutolewa Jumatatu (Februari 24 mwaka huu) kwenye ofisi za Idara ya Habari. Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Alhamisi (Februari 27 mwaka huu) saa 9 alasiri.
Ada kwa wagombea wa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mhazini na Mhazini Msaidizi ni sh. 50,000 kwa fomu. Nafasi za wajumbe wa Kamati ya Utendaji fomu zinapatikana kwa sh. 20,000.
Kamati ya Uchaguzi inawahimiza wanachama wa TASWA kujitokeza kwa wingi kugombea, lakini vilevile waisome vizuri Katiba ya chama chao.
Boniface Wambura
MWENYEKITI KAMATI YA UCHAGUZI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...