Wadau mbali mbali wa mchezi wa Soka jijini Dar es Salaam,leo wamekutana pamoja kwenye viwanja vya Tabata Shule katika Bonanza la kumuenzi Marehemu Omary Changa (pichani) aliyewahi kuwa Mchezaji katika timu za Yanga,JKT Ruvu,Kagera Suger pamoja na Moro United aliefariki dunia mwezi uliopita.Bonanza hilo limefanyika maalum kwa ajili ya kuchangisha fedha za kuisaidia familia ya Marehemu Changa ikiwa ni pamoja na kuweza kufanikisha kisomo cha Arobaini yake.
Mshambuliaji wa Pembeni wa timu ya Kijitonyama Veterans,Majuto Omary akichanja mbuga katika lango la wapinzani wao ambao ni Tabata Veterans,wakati wa Bonanza la kumuenzi Marehemu Omary Changa (pichani) aliyewahi kuwa Mchezaji katika timu za Yanga,JKT Ruvu,Kagera Suger pamoja na Moro United aliefariki dunia mwezi uliopita,lililofanyika leo kwenye Uwanja wa Tabata Shule,jijini Dar es Salaam.
hapiti mtu hapa.......
Beki wa Kati wa timu ya Kijitonyama Veterans akiondoka na mpira huku mpinzani wake akimsindikiza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...