Bango linalo onesha warsha ya kwanza ya Wadau wa Mfuko wa Misitu Tanzania
 Wadau mbalimbali wa Misitu wakiwa katika warsha hiyo mjini Morogoro 


Mfuko wa Misitu Tanzania ni Mfuko wa hifadhi ambao umeanzishwa kisheria kama njia endelevu ya kuwezesha uhifadhi wa rasilimali za misitu hapa nchini.Mfuko huu umeanzishwa kwa lengo la kukabiliana na changamoto za usimamizi wa rasilimali za misitu hasa katika kuimarisha utekelezaji wa Sera na Sheria ya Misitu.



Mfuko ilianza kazi rasmi Julai 2011.Mfuko wa Misitu Tanzania ni wa Umma na unasimamiwa na Bodi ya Wadhamini.Katika utendaji wa kila siku,Bodi ya Wadhamini inasaidiwa na Sekretarieti.

Mfuko wa Misitu Tanzania unafanya shughuli zake maeneo yote ya Tanzania Bara ambapo hutoa ruzuku kwa wadau wote wanojihusisha na usimamizi wa rasilimali za misitu na uboreshaji wa hali ya maisha ya wananchi waishio pembezoni wa misitu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...