Bunge nchini Kenya limepitisha sheria
inayomruhusu mwanaume kuoa wake wengi atakavyo, na halazimiki kumshauri mke
wake juu ya uamuzi huo.
Katika marekebisho ya Sheria ya Ndoa
ya Kenya yaliyopitishwa Alhamisi iliyopita, hata hivyo ndoa zote zitatakiwa
kusajiliwa na umri wa chini wa mwanamke kuweza
kuolewa umewekwa ili kuzuia ndoa za mapema za watoto, hasa wasichana.
Siku hiyo ya Alhamisi Wabunge wote
wanaume, ambao ni wengi, waliunga mkono kuondolewa kwa kipengele katika Sheria
hiyo ya Ndoa kilichomtaka mwanaume afanye mashauriano na mkewe kwanza kabla ya
kuoa mwanamke mwingine.
Wabunge wanawake waliolaani hatua
hiyo walikuja juu na kususia kikao kwa kutoka nje wakidai Sheria hiyo
haiwatendei haki wanawake



So very STUPID law, what message are they sending to the young girls and boys, what about allowing a woman to marry several husbands.
ReplyDeleteUKIMWI afilika hautaisha kamwe,
SHERIA HAIWATENDEI HAKI WANAWAKE WALIOKO KWENYE NDOA LAKINI INAWATENDEA HAKI WALE WASIOKUWA KWENYE NDOA NA WANATAKA KUOLEWA HATA KAMA NI MKE WA PILI.
ReplyDeleteNGOJA NIFANYE JITIHADA NIHAMIE KENYA.
Watumwa wa wazungu. Yaani kwa sababu mzungu ataka mke mmoja basi na sisi weusi lazima iwe hivyo.
ReplyDeleteSisi tuna tamaduni mila na desturi zetu bwana.
Nyie kina clementina endeni huko, sis Lawino watutosha.
KENYA SI NCHI YA KIDINI
ReplyDeletekwenye nchi ya kisekyula sheria ya mke mmoja (ya kikristo) haitakiwi ifatwe na wasio wakristo (wakabila na waislamu). Na mkristo ana haki ya uhuru wa kuoa mke mmoja halazimishwi kuoa wengi.
Nadhani haki imetendeka.
kwenye dini yetu ya kiislam mwisho wake wane sasa Kenya mbona hamjatuwekea wazi mwisho wake wangapi kuowa bila kushauriana wa mama watoto.
ReplyDeletekama zaidi ya wanne basi mtuletee habari upesi tupate kuhamia huko kwani hawatutoshi lakini katika dini sio katiba hamna mabadiliko.
HAPO WAKENYA KWELI WAJITAMBUA; HAWATAKI KUBURUZWA NA WAKOLONI. KWA MWENDO HUU MTAENDELEA KWA KASI, MUNGU AWASAIDIE. NA SASA MUNAJUA NINI MAANA YA KUWA BINADAMU, AHSANTE SANA
ReplyDeleteHawa warukia mambo wanachosha sana!!... hivi mmeelewa vizuri?? swala sio udini hapa, swala ni mwanaume kuongeza mke bila kushauriana na mama watoto kama ilivyokuwa awali, au??
ReplyDeleteHiyo ndiyo haki, kama alivyosema anony hapo juu "HAKI IMETENDEKA"
ReplyDeleteMKE WA MWANZO ASIULIZWE BALI ATAARIFIWE.
ReplyDeleteyaani mke wa kwanza akikataa basi jamaa asioe?
Swala hapa ni 'bila kushauriana na mkewe" ina maana polygamy ilikuwa inaruhusiwa toka zamani isipokuwa kwa ruhusa ya mke.
ReplyDeleteHaki za wanawake hapa hazipo / zimevunjwa.
Je mwanamke ana haki kuwa na uhusiano nje ya ndoa?
tusubiri katiba mpya ya Tanzania itatoa haki zipi kwa wanawake wa Tz,au watabakia kuwa "second class" kwenye sosait yetu?