Meneja Mkuu wa kampuni ya Global Publishers Ltd, Abdallah Mrisho, akielezea mchakato wa kumpata 'Mwanamke wa Mwaka' utakavyokuwa. Kushoto ni Mratibu wa Matukio wa Global Publishers, Luqman Maloto.
Wanahabari wakiwa kazini.
Luqman Maloto akisistiza jambo kwenye mkutano huo.

KAMPUNI ya Global Publishers Ltd ambao ni waandaaji wa shindano la kumtafuta mwanamke bora wa mwaka ambaye mchango wake wa maendeleo kwa jamii umewazidi wenzake, imethibitisha fainali hizo kufanyika keshokutwa Jumamosi.
Akizungumza na wanahabari kwenye Hoteli ya Atriums, Jijini Dar es Salaam, Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Abdallah Mrisho, amesema fainali hiyo itafanyika mjini Dodoma ambapo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye atawakabidhi tuzo washiriki wanne walioingia fainali na kumkabidhi tuzo maalum mmoja kati yao aliyewazidi wenzake alioingia nao fainali.
Washiriki walioingia fainali ni Prof. Anna Tibaijuka, Dk. Asha-Rose Migiro, Anna Kilango Malecela na Dk. Maria Kamm.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL )

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Hahaaaa...nyie wanaume mna mambo sana......ngoja na sisi wanawake tufanye mchakato wa kumtafuta MWANAUME WA MWAKA!

    ReplyDelete
  2. liwekwe shindano la mwanamke wa mwaka asiye mwanasiasa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...