Moja ya kero kubwa hapa Dar ni msongamano unaotokana na kutopangilia miundombinu na huduma vizuri. Kwenye magazeti ya siku za karibuni, imeripotiwa kuwa mpango wa kujenga stendi ya mabasi yaendayo mikoani eneo la Mbezi Luis umekwama kwa sababu eneo lile halifai kutokana na kuwepo mkondo wa maji. 
 Nimekuwa najiuliza kwa nini kujengwa stendi pale mahali hajapapimwa (hivyo ni vigumu kujengwa huduma za mahoteli, nk na kumwaga maji taka)... wakati mbele kidogo tu pale Luguruni kuna eneo kubwa limetengwa kuwa satellite city na mpaka sasa limebaki pori?
Kujenga hapo stendi kuu ya mabasi ya mikoani pamoja na soko kubwa la jumla kungetosha kuhamasisha uwekezaji ambao ndio ungesaidia patumike kama kituo cha huduma kama ilivyokusudiwa na kupunguza msongamano mji mkongwe wa Dar. 
Dar City Council bado wanatafuta maeneo kuweka hiyo stendi wakati Luguruni iko pori kubwa pale. Hata waliwahi kutaka kujenga stendi ya muda pale Chuo Kikuu Dar.
   Hivi humu hakuna anayehusika na haya mambo atuelimishe?
Mdau wa Mbezi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...