Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Bw. Andrii Deshchytsia akiwasilisha mbele ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Azimio ambalo pamoja na mambo mengine limeitaka Jumuiya ya Kimataifa na Mashirika ya Kimataifa, kutoitambua kura ya maoni iliyopigwa March 16 ya kujitenga kwa Crimea kutoka Ukraine na hatimaye kujiunga na Urusi, Ukraine inasema kura hiyo ya maoni si halali na ni njama za kumega mipaka halali ya nchi yake. Azimio hilo lilipitishwa siku ya Alhamis kwa kura 100 za ndiyo, 11 za hapana na 58 hazikuegemea upande wowote.
Muwakilishi wa Kudumu wa Urusi katika Umoja wa Mataifa, Balozi Vitaly I. Churkin akitoa maelezo kuhusiana na Azimio hilo lilowasilishwa na Ukraine na kuungwa mkono na nchi nyingi za Magharibi na zile za Ulaya, kwamba, kujitenga kwa Crimea kulikuwa halali na Urusi haikuwa na namna nyingine bali kuitambua kura hiyo na kusisitiza kwamba kihistoria Crimea ni sehemu ya Urusi.
Na Mwandishi Maalum
Wakati hali ya sintofahamu ikiendelea kuwa tete kufuatia Crimea kuamua kupiga
kura ya maoni na hivyo kujitenga kutoka Ukraine na kasha kujiunga na Urusi.Baraza
Kuu la Umoja wa Mataifa, jana alhamisi, limepiga kura kupitisha na kuunga mkono
azimio ambalo pamoja na mambo mengine, linaitaka Jumuiya ya Kimataifa kuto
tambua kwa namna yoyote iile kura hiyo na kujitenga kwa Crimea kutoka Ukraine.
Kabla ya tukio la upigaji kura kufanyika, baadhi ya wajumbe wanaoziwakilisha nchi
zao, walitoa maelezo ya kwa nini nchi zao zilikuwa zimeamua kupiga kura ya ama
kuunga mkono azimio , kutoliunga mkono au kutoegemea upande wowote.
Baada ya maelezo hayo, matokeo ya kura yalikuwa ifuatavyo, Nchi 100 zilipiga kura
ya ndiyo, nchi 11 zikipiga kura ya kulikataa azimio wakati nchi 58 zenyewe ziliamua
kupiga kura ya kutoegemea upande wowote.
Azimio hilo liliwasilishwa mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, na
Bw. Andrii Deschcytsia, Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine ambaye katika
uwasilishaji wake alijenga hoja zilizowataka wajumbe kuliunga mkono azimio hilo.
Naye Muwakilishi wa Kudumu wa Urusi katika Umoja wa Mataifa, Balozi Vitaly I.
Churkin yeye pamoja na kutetea uamuzi wa serikali yake wa siyo tu kutambua kura
hiyo ya maoni lakini pia kujitenga kwa Crimea, alitoa hoja ya kutaka upigaji wa kura
hiyo uwe ni wa kura zilizohesabiwa ( recorded vote).
Balozi Churkin alisititiza kwamba, kura ya maoni iliyopigwa na wananchi wa Crimea
na hatimaye kuamua kujitenga na kisha kujiunga na Urusi ilikuwa ni ni kura halali na
kwamba Urusi haikuwa na namna nyingine zaidi ya kuitambua kura hiyo.
Aidha kupitia azimio hilo ambalo limepitishwa baada ya Baraza Kuu la Usalama
kushindwa kupitisha azimio kama hilo mnamo March 15 siku moja kabla ya kura ya
maoni kufanyika baada ya Urusi kulipinga, linayataka pia Mashirika ya Kimataifa
kuto tambua kujitenga kwa Crimea na jiji la Sevastopol kwa mujibu wa kura ya maoni
ya March 16.
Ingawa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, limepitisha azimio hilo, azimio linakosa
nguvu kama ambavyo lingepitishwa na Baraza Kuu la Usalama.
Wengi wa wazungumzaji waliounga mkono azimio hilo, au hata wale ambao
hawakuegemea upande wowote,wamesisitiza haja na umuhimu wa kuheshimu Katiba
ya Umoja wa Mataifa pamoja na Misingi ya sheria za kimataifa, ambazo pamoja na
mambo mengine zinasisitiza kuheshimiwa kwa mipaka ya nchi na kutoingilia mambo
ya ndani ya nchi nyigine, pamoja na kuimarisha umoja na mshikamano.
Baadhi ya wazungumzaji, wameleezea wasiwasi wao kuhusu kupitishwa wa azimio hilo
ambalo limeungwa mkono karibu na nchi zote za Magharibi na zile za Ulaya kuwa
kwa kufanya hivyo ni sawa na kuchochea zaidi mgogoro huo.
wamarekani wamepata mtemi wao mara hii, wao wamezoea kuingilia nchi za watu ziko maelfu ya maili mbali na nchi yao kama iraki na afaganistani , sasa huyu nendeni mkapigane nae kama mna ubavu , mmebakia kuweka vikwazo vya uchumi , wakati mrusi huyo huyo mnamtumia akupelekeeni wanaanga wenu juu. Ubavu wa marekani kuonea nchi za kinyonge tu , mjaribuni basi na mrusi tuone nani mbabe ili tujue
ReplyDeleteKutokana na siasa za kimataifa za siku hizi inabidi ile Jumuia Ya Nchi Zisizofungamanga na Upande wowote(Non-Aligned Nations) ifufuliwe.
ReplyDeleteMdau
Christos Papachristou
Diaspoara
Ndugu yangu wa kwanza hapo juu, jua hamna nchi yenye ubavu wa kum piga mmarekani kivita just so u know. Russia they are not as powerful as they being portrayed to be! Get it right ndugu yangu! What happen in Crimea is not a threat to the world like what it was in Afghanistan na Iraq na hamna ukiukwaji wa haki za binadamu na uteswaji wa watu, Russia wamevuka mpaka tuu. That's the issue Kama umefuatilia sana au hata kidogo ungejua haya. Mdau Tabata.
ReplyDelete