Kikosi cha Kagera Sugar

Na Faustine Ruta, 
Bukoba
Ligi Kuu Vodacom imeendelea leo na hapa Mjini Bukoba tukishuhudia Timu ya Maafande kutoka Jijini Mbeya ikinyukwa bao 2-1 na  wenyeji Kagera Sugar katika uwanja wa Kaitaba. 
Kipindi cha kwanza Tanzania Prisons ndio walipata bao kupitia kwa mchezaji wao Peter Michael katika dakika ya 37 baada ya kuwachambua kama karanga mabeki wa Kagera Sugar na kuachia shuti kali na kumfunga kipa wa Kagera Sugar. 
Mpaka dakika za mapumziko Tanzania Prisons ndio wameenda kupumzika wakiwa mbele ya Bao 1-0 dhidi ya Wenyeji Kagera Sugar.Kipindi cha pili dakika ya 55 Kagera Sugar walipata penati na mkwaju huo ulipigwa na Salum Kanoni na kupata bao la kusawazisha. 
Katika dakika za lala salama dakika ya 88 Kagera Sugar walipata bao la ushindi lililofungwa na Benjamini Asukire kwa shuti kali ndani ya eneo hatari la penati nakufanikisha Timu yao kuibuka na ushindi wa bao hizo mbili.
Kikosi Cha Timu ya Tanzania Prisons kilichoanzaWaamuzi wa Mtanange huu wa Kagera Sugar na Tanzania Prisons ya jijini Mbeya
Kipute kimeanza kipindi cha kwanza...

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...