Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Wilayani Mufindi,Ndugu Miraji Mtaturu akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kwa tiketi ya chama hicho,Ndugu Godfrey Mgimwa mapema leo jioni mbele ya wanakijji cha Mfukulembe,(hawapo pichani),kata ya Ifunda,Iringa vijijini mkoani humo.
Mgombea Ubunge Jimbo la Kaleta (CCM),Ndugu Godfrey Mgimwa akiwahutubia wakazi wa Kijiji cha Mabikimitali,kata ya Ifunda katika jimbo hilo,mkoani Iringa leo jioni.Godfrey amewaomba wananchi hao kumuamini na kumpa ridhaa ya kuwaongoza kwa kumoigia kura zote za ndiyo katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika machi 16 mkoani humo.
Mkutano wa hadhara wa kampeni ya uchaguzi wa Ubunge jimbo la Kalenga,kupitia chama cha Mapinduzi,wa kumnadi mgombea wa chama hicho ukifanyika leo jioni kwenye kijiji cha Mibikimitali,kata ya Ifunda Iringa Vijijini
Ndugu Mwampamba akimuombea Kura,Mgombea Ubunge jimbo la Kalenga,kupitia chama cha CCM,Ndugu Godfrey Mgimwa jioni ya leo katika kijiji cha Mibikimitali,kata ya Ifunda,Iringa Vijiini.
Baadhi akina Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni ya uchaguzi wa Ubunge jimbo la Kalenga,kupitia chama cha Mapinduzi,mapema leo jioni kwenye kijiji cha Mibikimitali,kata ya Ifunda Iringa Vijijini,ambapo mgombea wa chama hicho,Ndugu Godfrey Mgimwa ndiye amesimamishwa kwenye jimbo hilo kuomba ridhaa ya kuonngoza.
Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia mkutano huo.
Baadhi ya Wanakijiji cha Mibitimitali wakishangilia jambo
Baadhi ya Wadau wa CCM,wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano wa kampeni ya Uchaguzi,jimbo la Kalenga,Iringa vijijini,uliofanyika katika kijiji cha Mfukulembe,kata ya Mafinga,mkoani Iringa mapema leo jioni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...