Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akipokelewa kwa shangwe na Wanachama mbalimbali wa chama hicho mapema leo asubuhi alipokuwa akiwasili kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Ilala,ambapo alizungumza machache na  kamati ya siasa ya Wilaya na baadae kuanza ziara rasmi wilaya ya Ilala.

 Pichani kulia ni Mwenyekiti Mkoa wa CCM,Dar Es salaam Ndugu Ramadhan Madabida akizungumza jambo mbele ya kamati ya Siasa ya mkoa (hawapo pichani) mapema leo,kwenye ofisi Kuu za CCM mkoa,ambapo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana (pichani kushoto) anaanza rasmi ziara ya siku nne mkoani humo,ambapo atatembelea wilaya ya Ilala (ambayo ameianza leo),Temeke na Kinondoni. Lengo la ziara hiyo ikiwa ni kuimarisha chama cha CCM na kuhamasisha na kutenda utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi,sambamba na ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Pichani kulia ni Mwenyekiti Mkoa wa CCM,Dar Es salaam Ndugu Ramadhan Madabida akimkabidhi Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana taarifa ya hali ya kisiasa mkoani Dar es salaam,mapema leo mara baada ya kufanyika kikao kifupi cha kuanza ziara ya siku ya nne mkoani humo
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza kwenye kikao kifupi mbele ya kamati ya Siasa ya mkoa mapema leo,kwenye ofisi Kuu za CCM mkoa.Ndugu Kinana anaanza rasmi ziara ya siku nne mkoani humo,ambapo atatembelea wilaya ya Ilala (ambayo ameianza leo),Temeke na Kinondoni. Lengo la ziara hiyo ikiwa ni kuimarisha chama cha CCM na kuhamasisha na kutenda utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi,sambamba na ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
 Baadhi ya Wananchi wakiutazama msafara wa Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (haupo pichani),ulipokuwa ukiwasili kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Ilala

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...