Marehemu Rabbiel Daniel Swai 
(7/3/1941 – 3/3/1997)

Ni miaka kumi na saba (17) ya majonzi na huzuni imepita, tangu ulipo tutoka gafla katika maisha ya duniani, siku ya Jumatatu na tarehe kama hii 3 March 1997.

Kama wakristo tunaamini, maisha ni safari na mungu ndiye aliyeamua kuwa wewe upumzike mapema.  Pamoja na kuwa umetutoka kimwili, ki roho bado uko nasi.

Unakumbukwa sana na mkeo mpendwa wako Elly Rabbiel Swai,  watoto wako  wapendwa Doris, Nelson, Clemence, Frank na Edward. Wakwe zako  Aikael , Gloria na Tutu.

Wajukuu zako Bradley, Dryden, Deryne, Desmond, Donavan na Ellie Reney bila kuwasahau dada yako Elly Ndosi , ndugu zako wote, jamaa na marafiki wote waliokupenda kwa moyo.

Hakika tunakukumbuka kwa mema mengi  uliyotuachia, haswa upendo wa dhati kwa wote, tukiamini ndio taa itumulikayo katika maisha yetu.

Tunamshukuru mungu kwa zawadi ya maisha yako, na kwa miaka mingi ya Baraka tuliyo kuwa pamoja hapa duniani. Tunakuombea mungu baba akupe mapumziko mema  mpaka pale tutakapo kutana tena.

Tunakumbuka faraja tunayoipata katika Zaburi ya 123.

Amen.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...