MSHAURI Mkuu wa Ufundi wa Wakala wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART), Bwana Dieter Schelling (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (ambao hawapo pichani) eneo la Kimara kuwa Kampuni ya STRABAG kuruhusu vituo tano vitumike kugeuzia magari (U-turns) mpaka vituo vya kudumu vitakapokamilika ndani ya miezi sita. Kushoto ni Mhandisi wa DART, Mhandisi John Shauri.
Sehemu ya barabara ya Morogoro
road maeneo ya Kimara
KAMPUNI ya ujenzi wa barabara ya STRABAG inayoendelea na ujenzi kwa ajili ya mradi wa mabasi yaendayo haraka umeruhusu upande mmoja wa barabara uliokamilika kutumika ili kupunguza foleni ya magari yanayoka Kimara kuelekea katikati ya jiji au sehemu nyingine kupitia
barabara ya Morogoro. road maeneo ya Kimara
Mhandisi
wa Wakala wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART),Mhandisi John Shauri
aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kwamba
mbali ya kuruhusu upande mmoja wa barabara, kampuni ya STRABAG imeruhusu pia
vituo vitano vitumike kwa kugeuzia magari kwa muda wa miezi sita (provisional
U-turns) mpaka maeneo matatu ya kudumu yatakapo kamilika katika kipindi hicho.
“Kuruhusu
upande mmoja kutumika na pia maeneo ya kugeukia magari kumesaidia sana
kupunguza foleni kwa magari yanayotoka kimara kwenda Ubungo nay ale yanayotoka
Ubungo kwenda Kimara,”alisema Mhandisi Shauri.
Mhandisi
huyo amewataka madereva kuwa waangalifu na mwendo kwani wastani wa mwendo
unaotakiwa ni spidi 50 tu na si vinginevyo kwani mwendo kasi utasababisha ajali
zisizo za lazima.
“Mwendo
wa kawaida utasaidia sana maeneo ambayo yameruhusiwa magari kugeuka na na kuelekea
sehemu husika bila kusababisha ajali,” alisema na kuongeza kuwa mradi
utakapokamilika utapunguza kabisa foleni na msongamano wa magari.
Mhandisi
Shauri ambaye aliambatana na Mshauri Mkuu wa Ufundi wa Mradi huo, Bwana Dieter
Schelling, alivitaja vituo hivyo vitano vya kugeuzia kuwa ni Kimara
Corner,Kimara Baruti, katikati ya Kimara Butcher na Kimara kwa Thomas, Kimara
Resort na Kimara mwisho.
“Kwa
sasa magari katika barabara hii ya Morogoro magari yanapita pasipo msongamano
mkubwa kama ilivyokuwa awali na kurahisisha watu kutoka Mbezi,Kibamba kuwahi
kwa wakati katika shughuli zao,” alisisitiza mhandisi Shauri.
Amesema
wakati ujenzi ukiwa unaendelea vyema daladala zingeendelea kupita/kutumia
barabara za pembeni (access roads) badala ya kutumia barabara kubwa kwani
itapunguza sana msongamano.
“Katika
kipindi hiki usimamiaji wa zoezi hili linahitaji kuungwa mkono na askari wa
barabarani ilikuwadhibiti madereva wote wanaotembea kwa mwendo kasi
ilikupunguza ajali ambazo zinaweza kuepukika.
Kwa
mujibu wa mhandisi Shauri, vituo vya kudumu vya kugeuzia (permanent U-turns)
vitajengwa Kimara Baruti, Kimara Butcher na Kimara Mwisho.
Mradi
huo mkubwa wa ujenzi unasimamiwa na Wakala wa Usimamizi wa Barabara nchini
(TANROADS). DART ipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa (TAMISEMI).
Hivi
karibu waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli alifanya ziara ya kukagua maendeleo
ya ujenzi wa barabara ya mradi wa mabasi
yaendayo haraka ambapo aliridhishwa na maendeleo ya ujenzi unaofanywa na
kampuni ya STRABAG kutoka ujerumani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...