Na Abdulaziz Video, Kilwa
Moto umeteketeza nyumba anayoishi mkuu wa wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi, Mhe. Abdallah Ulega na kusababisha hasara kubwa ambayo idadi yake haijaweza kufahamika mara moja. 
 Habari kutoka wilayani humo na kuthibitishwa na Katibu tawala wa mkoa wa Lindi  Bw. Abdala Chikota alisema kwamba moto huo umeteketeza vifaa mbalimbali  ndani ya nyumba ya kiongozi huyo. 
 Bw. Chikota alisema moto huo umesababisha hasara kubwa. 
 Alisema kufuatia tukio hilo ofisi ya mkuu wa mkoa imetoa fedha Shilingi laki tano 500.000 pamoja na chakula kama mchele, unga sukari, mafuta ya kula pamoja na maharage ili kumsaidia DC huyo  katika kipindi hiki cha majonzi wakati  utaratibu mwingine wa kutatua tatizo la makazi yake ukifanyiwa kazi.
Mkuu wa wilaya huyo, Mhe. Ulega, alisema kuwa vitu vichache tu ndiyo vimeweza kuokolewa, ambavyo vilikuwa rahisi kuchukuliwa ikiweno begi la nguo na nyaraka zake, na kwamba kwa sasa atalazimika kuishi katika jengo la Hostel. 
 Mhe. Ulega ameshukuru  juhudi za wananchi ambazo zimesaidia kuokoa vitu vichache, vikiwemo seti ya makochi, magodolo matatu na kitanda kimoja cha mbao
Amesema wakati nyumba yake ilipokuwa ikiungua, familia yake akiwemo mke alikuwa safarini na amerejea leo mchana.
  Kwa upande wake kamanda wa polisi Regnal Mzinga amethibitiasha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi unafanyika ili kubaini chanzo cha moto huyo
mkuu wa wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi, Mhe. Abdallah Ulega (mwenye tracksuit ya bluu) na majirani wakiwa nje ya nyumba yake iliyoteketea kwa moto asubuhi ya leo
Sehemu ya uani mwa nyumba hiyo
Sehemu ya ndani
Nyumba hiyo kwa mbele
Sehemu ya ndani ya nyumba hiyo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Haya matukio ya moto yamezidi, kama yakizidi tutahitaji kuwa na fire extinguisher kila nyumba sasa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...