Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule akisalimiana na Mhe. Tanja Rasmusson, Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Kimataifa wa Sweden alipofika Wizarani leo. Mhe. Rasmusson yupo nchini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili. Katika mazungumzo yao waligusia masuala ya kuimarisha ushirikiano katika nyanja za biashara, uwekezaji, elimu, haki za binadamu na vita dhidi ya rushwa.
Mhe. Rasmusson akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Wizarani.
Wajumbe waliofuatana na Mhe. Rasmusson wakifuatilia mazungumzo kati ya Bw. Haule na Mhe. Rasmusson (hawapo pichani). Wa kwanza kulia ni Balozi wa Sweden hapa nchini, Mhe. Lennarth Hjelmaker.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...