Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Irina Bokova, ( kati kati) akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu Teknolojia ya habari na mawasiliano na mchango wa vyombo huru vya habari katika kuwawezesha wanawake na watoto wa kike, katika majadiliano hayo, wazungumzaji waliokaa meza kuu ambao ni kutoka kushoto, Bi. Elisa Munoz, Mkurugenzi Mtendaji wa IWMF, Muwakilishi wa Kudumu wa Austria Balozi Martin Sjdik, Bw. Peter Launsky-Tieffenthal Katibu Mkuu Msaidizi na mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya Umma ya Umoja wa Mataifa , Anne Bennett, Mkurugenzi Mtendaji wa Hirondelle ( USA) na Pamela S. Fall, anayeripoti katika kituo cha CBS na Rais wa chama cha Waadishi wa habari Umoja wa Mataifa walijadili kwa kina umuhimu wa teknolojia ya habari na mawasiliano kama nyezo muhimu ya uwezeshaji wa wanawake na watoto wa kike, lakini pia kama nyezo muhimu katika kuwapatia habari na taarifa mbalimbali, habari zinazoandaliwa na vyombo huru na ambavyo waandishi wake wenyewe na weledi wa matumizi ya ICT.
sehemu ya washiri wa majadiliano kuhusu ICT ambayo yaliandaliwa kwa pamoja na UNESCO na Uwakilishi wa Kudumu wa Austria na kufanyika sambamba na mkutano wa 58 wa Kamisheni kuhusu Hali ya Wanawake. katika majadiliano hayo, Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya International Women's Media Foundation, (IWMF mwenye suti nyekundu, alitoa taarifa kuhusu uzinduzi utakaofanywa wa ripoti ya utafiti kuhusu mazingira hatarishi wanayofanyia kazi waandishi wa habari wanawake. Ripoti hiyo yenye kurasa 40 inahusu utafiti uliofanywa kwa kuwashirikisha waandishi wa habari wanawake 1,000 kutoka duniani kote.
Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bibi. Anna T. Maembe, akifutilia majadiliano ambayo yameingia siku ya pili ya ajenda kuu ya Mkutano wa 58 wa Kamisheni kuhusu Hali ya Wanawake, ajenda hiyo ni mafanikio na changamoto za utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Millenia, ( MDGs) kwa wanawake na watoto wa kike. Mkutano wa 58 wa CSW ulifunguliwa siku ya jumatatu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...