Na Lorietha Laurence-Maelezo

Asilimia 1.03 ya vifo hutokana na ugonjwa wa figo, hayo yalisemwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii  Seif Rashidi alipokuwa akitoa tamko kwa waandishi wa habari  leo jijini Dar es salaam,kuhusu siku ya afya ya figo itakayoadhimishwa  tarehe 13 Machi,mwaka huu mjini Dodoma.

 Kauli mbiu ya maadhimisho hayo “Figo huzeeka, kadiri mtu anavyozeeka. Jali Afya ya Figo zako”. Lengo ni  kuelimisha  jamii ili iweze kuelewa umuhimu wa  figo katika   mwili, watu kubadili staili za maisha, kuhamasisha  watoa huduma kuhusu wajibu wao katika kugundua magonjwa ya figo na kupunguza hali hatarishi za ugonjwa sugu wa figo na kuandaa mikakati madhubuti ya kukinga na kuthibiti magonjwa ya figo.

“ Nawasihi watu wawe na taratibu za kufanya vipimo mara kwa mara, pia kujali afya zao kwa kuwekeza katika maendeleo ya afya zao ili kujikinga na ugonjwa wa figo” alisema Mhe.Rashidi .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...