Na Lorietha Laurence-Maelezo
Asilimia 1.03 ya vifo hutokana na ugonjwa wa figo, hayo yalisemwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Seif Rashidi alipokuwa akitoa tamko kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam,kuhusu siku ya afya ya figo itakayoadhimishwa tarehe 13 Machi,mwaka huu mjini Dodoma.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo “Figo huzeeka, kadiri mtu anavyozeeka. Jali Afya ya Figo zako”. Lengo ni kuelimisha jamii ili iweze kuelewa umuhimu wa figo katika mwili, watu kubadili staili za maisha, kuhamasisha watoa huduma kuhusu wajibu wao katika kugundua magonjwa ya figo na kupunguza hali hatarishi za ugonjwa sugu wa figo na kuandaa mikakati madhubuti ya kukinga na kuthibiti magonjwa ya figo.
“ Nawasihi watu wawe na taratibu za kufanya vipimo mara kwa mara, pia kujali afya zao kwa kuwekeza katika maendeleo ya afya zao ili kujikinga na ugonjwa wa figo” alisema Mhe.Rashidi .
Asilimia 1.03 ya vifo hutokana na ugonjwa wa figo, hayo yalisemwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Seif Rashidi alipokuwa akitoa tamko kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam,kuhusu siku ya afya ya figo itakayoadhimishwa tarehe 13 Machi,mwaka huu mjini Dodoma.
Kauli mbiu ya maadhimisho hayo “Figo huzeeka, kadiri mtu anavyozeeka. Jali Afya ya Figo zako”. Lengo ni kuelimisha jamii ili iweze kuelewa umuhimu wa figo katika mwili, watu kubadili staili za maisha, kuhamasisha watoa huduma kuhusu wajibu wao katika kugundua magonjwa ya figo na kupunguza hali hatarishi za ugonjwa sugu wa figo na kuandaa mikakati madhubuti ya kukinga na kuthibiti magonjwa ya figo.
“ Nawasihi watu wawe na taratibu za kufanya vipimo mara kwa mara, pia kujali afya zao kwa kuwekeza katika maendeleo ya afya zao ili kujikinga na ugonjwa wa figo” alisema Mhe.Rashidi .
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...