Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Bibi. Anna T. Maembe akisisita haja na umuhimu wa wazazi kuwawezesha watoto wao wa kike kuyapenda masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hesabu ( STEM) badala ya kuliachia jukumu hilo serikali au walimu. Alikuwa akizungumza katika mkutano wa pembezoni ulioandaliwa kwa pamoja kati ya Tanzania, Uingereza na Kampuni ya Kimataifa ya GlaxoSmithkline ili kujadili fursa na changamoto za mwanafunzi wa kike katika masomo hayo, kulia kwa Katibu Mkuu ni Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Bibi. Irina Bokova ambaye alikuwa modereta wa majadiliano hayo na pia alielezea nafasi na Mchango wa UNESCO katika kumsaidia mtoto wa kike. Kushoto ni Balozi Ramadhan Mwinyi , Naibu Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Wizara ya Wanawake na Usawa wa Uingereza, Bibi, Maria Miller ( Mb) akielezea uzoefu wa nchi yake katika kuwahamasisha watoto wa kike kupenda masomo ya STEM, kulia kwake ni Bibi Nicola Yates, Makamu wa Rais wa UK and Ireland Phamarceuticals na Meneja Mkuu wa GlaxoSmithkline. Nyuma ya Waziri Miller na anayefuatilia kwa makini majadiliano hayo ni Mwanamitindo Bi. Flaviana Matata ambaye pamoja na kujikita fani ya mitindo na ambayo imemjengea heshima kubwa, lakini pia kupitia Taasisi yake ya Flaviana Matata Foundation ameonyesha mapenzi makubwa ya kuwasaidia wanafunzi kuipenda shule na kudumu shuleni.
Makatibu Wakuu kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bibi. Asha Ali Abdullah ( Wizara ya Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto) na Bibi. Mwanaidi Salehe Abdulla ( Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amari) wakifuatilia majadiliano hayo kuhusu fursa na uwezeshaji wa wanafunzi wa kike kujiunga na masomo ya sayansi, teknolojia, uhandisi na hesabu.
sehemu wa washiriki wa Mkutano wa 58 wa Kamisheni kuhusu Hali ya Wanawake, walioshiriki majadiliano hayo ambapo pia walipata fursa ya kuchangia kwa kuuliza maswali meza kuu iliyowahusisha Katibu Mkuu, Anna Maembe, Mkurugenzi Mkuu UNESCO, Irina Bokova, Waziri Maria Miller ( Mb) na Nicola Yates Meneja Mkuu GlaxoSmithkline ambao ndio waliokuwa wazungumzaji wakuu.
Wazazi wanaweza kushauri watoto wao lakini jitihada za shule kupatiwa walimu wazuri na maabara ni muhimu zaidi.
ReplyDelete