Gari ya Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam,Meck Sadicky likinasuliwa kwenye tope baada ya kukwama katika kijiji cha Mataya-Ruvu Chini,yote hiyo ikiwa ni sehemu ya changamoto ya Miundo mbinu hasa barabara,Wakati wakiongoza msafara wa Katibu MKuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa anakwenda kukagua chanzo cha Maji Ruvu chini na kujionea upanuzi wa chanzo hicho mapema jana jioni;wakati Ndugu Kinana alipokuwa akihimitimisha ziara yake ya siku tatu ndani ya wilaya ya Kinondoni,ziara hiyo ikiwa na lengo la Kuimarisha uhai wa chama cha CCM na kukagua miradi mbalimbali ikiwa ni sehemu utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi 2010.
Utaratibu wa kulinasua ukiendelea.
OOppss..haya twendeeeee....!
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam,Mh.Mecky Sadicky akimfafanulia jambo Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana,mara baada ya kukumbana na changamoto ya miundombinu,wakati wakielekea kukagua chanzo cha Maji Ruvu chini na kujionea hali halisi na kazi kubwa inayofanyika ya upanuzi wa chanzo hicho mapema jana jioni,wakati Ndugu Kinana alipokuwa akihimitimisha ziara yake ya siku tatu ndani ya wilaya ya Kinondoni,ziara hiyo ikiwa na lengo la Kuimarisha uhai wa chama cha CCM na kukagua miradi mbalimbali ikiwa ni sehemu utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi 2010.
Wakitafakari namna ya kupita mara baada ya kukutana na changamoto ya miundombinu,hasa barabara kama uonavyo pichani Lori likiwa limeziba njia kutokana na hali ya mvua kunyesha eneo hilo.
PICHA ZAIDI INGIA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM.
PICHA ZAIDI INGIA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM.
Hii ni fundisho kwa viongozi wetu. Wameona jinsi wanachi wa maeneo hayo wanavyopata shida. Kazi kwake kuakikisha wanapata barabara inayopitika kwa nyakati zote za majira ya mwaka.
ReplyDeleteBarabara hii itengenezwe, Ukiona Prado imekwama ujue barabara hii ni mbaya.
ReplyDeleteAcha apate
ReplyDeleteCCM, CCM, CCM, CCM watatuzi wa changamoto zinazowakabili wananchi Tanzania.
ReplyDelete