Wiki
kama hii, miaka 20 iliyopita, nchi ya Rwanda ilishuhudia kuanza kwa
mauaji ambayo kwa siku 99 zilizofuata, yaliacha historia mbaya na ambayo
itaendelea kukumbukwa na vizazi vijavyo.
Ndani ya siku 100, watu wanaokadiriwa kufika milioni 1 waliuawa katika mauaji ya kimbari.
Miaka
20 baadaye (mwaka huu), dunia nzima imeungana na Rwanda kukumbuka kile
ambacho wengi wanaona kuwa kilitokea na kuachwa kuendelea kutokana na
Jumuiya ya kimataifa kutoingilia kati na kutoa msaada muafaka kwa wakati
muafaka.
Kumekuwa na matukio mbalimbali kukumbuka mauaji ya kimbari
ya Rwanda ambayo yamefanyika duniani kote, Kutoka Kigali Rwanda mpaka
hapa Dar-Es Salaam na hata huko Washington DC.
Hii ni sehemu ya
ripoti ya Kwanza Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA
kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam
Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).
Hii ilikuwa ripoti ya Aprili 12, 2014
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...