Janneth Emmanuel (kushoto),  Cresenciah Herman (katikati) na Joshua Wambura Stanslaus ambao ndio washindi wa Shindano la kusaka vipaji vya kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents wakiwa wanaonyesha zawadi zao za pesa taslimu shilingi laki 5 kila mmoja mara baada ya kutangazwa washindi wa Kanda ya Ziwa.
Shindano la Kusaka VIpaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents limemalizika leo kanda ya ziwa, Mkoani Mwanza kwa washindi watatu kupatikana na kupewa zawadi zao. Washindi hao ni Janneth Emmanuel , Cresenciah Herman  na Joshua Wambura Stanslaus huku binti mwenye umro mdogo kuliko washiriki wote Emiliana Fidelis mwenye umri wa Miaka 11 aliweza kung'ara kwa kuonyesha kipaji cha hali ya juu tokea mwanzo hadi Mwisho wa mashindano haya na kuweza kuvuta hisia za majaji na kupelekea majaji kumtangaza mshindi wa shindano hili lakini kutokana na Umri wake kuwa ni chini ya kigezo cha umri uliohitajika hatoweza kwenda Dar Es Salaam Kwaajili ya fainali lakini majaji hawakumuacha bure walimpatia zawadi za Shilingi laki Moja kama ishara ya yeye kuwa Mshindi pia.
Baada ya Mashindano haya kumalizika Kanda ya Ziwa Mkoani Mwanza sasa Zoezi linahamia Kanda ya Kati Mkoani Dodoma wiki hii ambapo Zoezi zima la usajili litafanyika kuanzi jumamosi ya tarehe 12 hadi 15 aprili  ambapo pia watatafutwa washindi watatu pia wa kanda ya kati.
Washindi hawa watatu wataungana na washindi wengine watakaopatikana katika kanda zingine katika fainali itakauofanyika Mkoani Dar Es Salaam Na mshindi kupata Zawadi kubwa ya Shilingi Milioni 50 za Kitanzania. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...