Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Ulongoni, Bi. Sikitiko Salehe,( wa pili kulia) akipokea moja ya madawati kati ya 93 kwa niaba ya shule yake kutoka kwa Mstahiki Meya Jerry Silaa ikiwa ni zao la matunda ya Mayor's Ball 2013 iliyoweka kipaumbele kwenye elimu kuhakikisha kila mwanafunzi anakaa kwenye dawati katika hafla fupi iliyofanyika kwenye shule ya sekondari Pugu jijini Dar.
Wanafunzi wa Shule ya sekondari Pugu wakionyesha nyuso za furaha isiyo na kifani walipokabidhiwa madawati 107 na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa.
Mstahiki Meya Jerry Silaa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa ngazi mbalimbali Kata za Gongo la Mboto na Pugu.
Mstahiki Meya Jerry Silaa akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa shule ya sekondari Pugu mara baada ya kukabidhi madawati 107 kwa shule hiyo.
Kaka mkuu wa shule ya Sekondari Pugu, Nicetas Ndekubali Ndeng'asso, akitoa shukrani kwa niaba ya wanafunzi wenzake kwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...