Utekelezaji wa OSBPs pamoja na kuandoa utaratibu wa sasa ambapo aina zote za udhibiti zinazofanyika mpakani hufanyika mara mbili, shughuli zote za udhibiti zitaendelea kufanyika kwa ukamilifu katika upande mmoja badala ya kulazimika kurudiwa katika upande wa pili wa mpaka kama ilivyo zoeleka.
Mradi huu unatekelezwa kwanza
kwa kutunga Sheria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya kuanzisha Vituo
Vya Utoaji Huduma Kwa Pamoja Mipakani (OSBPs) katika Nchi Wanachama wa Jumuiya
ya Afrika Mashariki. Tayari Bunge la Afrika Mashariki lilipitisha Sheria hiyo
mwezi Mei, 2013 na sasa iko katika hatua za kuidhinishwa na Wakuu wa Nchi
Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Hatua ya pili ni ujenzi wa
OSBPs hizo katika mipaka mbalimbali ambayo iko katika hatua zifuatazo:
Holili/Taveta mpaka
unaozitenganisha Tanzania na Kenya kwa upande wa Holili OSBP imekamilika na
imekabidhiwa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania ambao ndio waendeshaji wa OSBP zote
nchini na upande wa Kenya mpaka wa Taveta mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi
Mei, 2014.
Katika Mipaka ya Sirari/Isebania
unaozitenganisha Tanzania na Kenya kwa upande wa Mkoa wa Mara na Mpaka wa Mutukula/Mutukula unaozitenganisha Tanzania na
Uganda kwa upande wa Tanzania Vituo vimekamilika. Aidha, Ujenzi wa Kituo cha
Namanga ulioanza mwezi Desemba, 2011
kama sehemu ya Mradi wa barabara ya Arusha – Namanga – Athi River unaendelea.
Kituo cha Kabanga/Kobero kilichopo
katika mpaka wa Tanzania na Burundi muda wa Mradi ni miezi 15 na ulianza mwezi
Mei, 2013 na unatarajiwa kukamilika Juni, 2014, hatua ya ujenzi wake imefikia 20% hadi kufikia Februari, 2014.
Mradi wa ujenzi wa OSBP ya Rusumo
mpaka uliopo kati ya Tanzania na Rwanda umefikia asilimia 69.5% upande wa
Tanzania hadi kufikia mwezi Februari, 2014 na unatarajiwa kukamilika ifikapo
mwezi Novemba, 2014.
Mradi huu pia unatekelezwa katika
mpaka wa Horohoro/Lungalunga mpakani
mwa Tanzania na Kenya kwa upande wa Mkoa wa Tanga, ambapo hadi kufikia tarehe 31 Desemba, 2013 ujenzi wa kituo hiki
ulikuwa umekamilika 90% na ilitarajiwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Machi,
2014 Mradi kuwa umekamilika.
Kwa upande wa Tunduma OSBP
– kituo kinafadhiliwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Trade Mark East Africa (TMEA)
chini ya usimamizi wa TBA. Ujenzi bado haujaanza; TMEA wako katika mchakato wa
kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa jengo la OSBP.
Rasimu ya Mkataba wa Ubia (Bilaterall
Agreement) ya uendeshaji wa OSBPs kati ya Tanzania na Kenya imekamilika.
Taratibu za kusaini Mkataba huu zinakamilishwa ili usainiwe hivi karibuni na
kuwezesha Kituo kuanza kufanya kazi.
Ujenzi wa Vituo vya Utoaji Huduma kwa Pamoja Mipakani utasaidia usafiri na usafirishaji wa haraka kwa kuondoa urasimu mipakani na hivyo kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji kwa Wanaafrika Mashariki.
Ujenzi wa Vituo vya Utoaji Huduma kwa Pamoja Mipakani utasaidia usafiri na usafirishaji wa haraka kwa kuondoa urasimu mipakani na hivyo kupunguza gharama za usafiri na usafirishaji kwa Wanaafrika Mashariki.
![]() |
Mkurugenzi Udhibiti Ubora kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Bi. Tumaini Mtitu akiwaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam mikakati ya kudhibiti ubora wa bidhaa za ndani na zinazotoka nje ili kuepuka madhara kwa watumiaji wa bidhaa hizo. Kushoto ni Afisa Uhusiano wa shirika hilo Bi Roida Andusamile. |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...