Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akipanda mti eneo la jengo la utawala wa Chuo Kikuu cha Dodoma wakati alipotembelea chuoni hapo kwa ajili ya kufungua rasmi kongamano la Mustakabali wa mtoto wa kike katika mazingira ya sasa kwa wanafunzi wa kike wa vyuo vikuu vilivyopo Dodoma na Morogoro. Kongamano hilo lilifanyika katika ukumbi wa Chimwaga tarehe 12.4.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikaribishwa ukumbini na wanafunzi wa kike waliojawa na furaha na hamasa kubwa.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akishiriki kucheza kwa nderemo na vifijo na wanafunzi wa kike wa vyuo vikuu mbalimbali vya Dodoma na Morogoro wimbo uitwao ..”wanawake na maendeleo..” mara baada kuingia ukumbini. Mama Salma alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa kongamano la mustakabali wa mtoto wa kike katika mazingira ya sasa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...