ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani, Emmanuel Nchimbi anatarajia kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Pasaka linalotarajia kufanyika Aprili 26 Wilayani Songea mkoani Ruvuma.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama wakazi wa mkoa huo na maeneo ya jirani wajitokeze kwa wingi  kufanikisha sherehe ya kufufuka kwa mwokozi Wetu Yesu Kristo.
 Msama alisema mbali ya Nchimbi kuwa mgeni rasmi Songea, jijini Mbeya mgeni rasmi atakuwa ni Mbunge wa viti maalum, Mary Mwanjelwa  wakati mkoani Dodoma mgeni rasmi atakuwa mbunge wa Tarime, Nyambari Nyangwine. Aidha Msama alitoa fursa kwa wakazi wa mikoa litakapofanyika Tamasha la Pasaka kujitokeza kwa wingi ili kufanikisha ufanikishaji wa ujenzi wa Kituo cha Kimataifa cha wenye uhitaji Maalum cha Jakaya Mrisho Kikwete rafiki wa Wasiojiweza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...