Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimia wananchi wakati alipokuwa anaingi uwanja wa Uhuru leo katika maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar..Pembeni ni Mkuu wa majeshi Jenerali Davis Mwamunyange.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua vikosi vya ulinzi na usalama wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam leo.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Joyce Banda wa Malawi katika sherehe za miaka 50 ya Muungano.Rais Banda kwa sasa ndiye mwenyekiti wa jumuiya ya uchumi kusini mwa Afrika SADC.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais wa Zanzibar Dkt.Mohamed Ali Shein wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya muungano.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Mfalme MswatiIII katika sherehe za miaka 50 ya Muungano zilizofanyika katika viwanja vya uhuru leo.
Rais dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Yoweri Kaguta Museveni katika sherehe za miaka 50 ya Muungano.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi katika maadhimisho ya hsrehe za miaka 50 ya Muungano.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Uhuru Kenyatta katika hsrehe za miaka 50 ya Muungano.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Mohamed Ali Shein na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange wakiwa na viongozi wa nchi mbalimbali za Afrika kwnyesherehe za Miaka 50 ya Muungano katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo. Wengine toka kushoto ni Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi, Mfalme Mswati wa III
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal, Mfalme wa Lesotho na rais wa Malawi Dkt Joyce Banda. na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange wakiwa na viongozi wa nchi mbalimbali za Afrika kwnyesherehe za Miaka 50 ya Muungano katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal,  na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange wakishyangilia kwa furaha wakati Makomandoo wakishuka kwa miavuli uwanjani kama inavyoonekana hapo chini. Mapicha ya kumwaga baadae kidoooogo.... 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Tuekeeni video ili sisi tuliombali tuone mambo yalivyokuwa-SEOUL. South korea

    ReplyDelete
  2. I like that .."The Mighty JWTZ" wamewaonesha hao wanaocheza cheza na Tz kua wakijaribu wataisoma number....nashukuru Kaguta alikuwepo kwani atampelekea salaam PK..na Mama Banda yeye alishudia live..Hongera sana Mh. rais JK kwa kuliongoza taifa letu kwa umakini mkubwa na salaam zingine ziwafikie UKAWA huko waliko kwamba muungano utadumu milele...Ameen.
    Mdau wa UK

    ReplyDelete
  3. MAPINDUZI???? Nilidhani tunaadhimisha Muungano.

    ReplyDelete
  4. USITUCHANGANYE, SHEREHE HII SIYO YA MAPINDUZI NI SHEREHE YA MUUNGANO.

    ReplyDelete
  5. kweli bwana michuzi tuwekee clip tuone ss tulio mbali

    ReplyDelete
  6. Tunaomba hotuba ya tarehe 25 na 26 ya mheshimiwa rais jk

    ReplyDelete
  7. Tunaomba hotuba ya mheshimiwa rais ya muungano na ya tarehe 25

    ReplyDelete
  8. tunaomba hotuba zote tangu arusha, p.t.a saba saba, na taifa. pls nkali

    ReplyDelete
  9. Hongera JK kwa kuifikisha TZ yetu halo ilipo na kuwaonesha wale wenye chuki kuwa ukituchezea silaha na vijana wenye ari tunao. Kagame hakuwepo ila nadhani alikuwa anaangalia vijana wenye kofia nyekundu wakifanya maonesho. M23 inawatambua vyema Babu Museveni atakupa taarifa nzuri zaidi

    ReplyDelete
  10. TUNAOMBA HOTUBA YA 25TH APR

    ReplyDelete
  11. Mapidnuzi na Muungano ni kama CHAI NA MKATE!

    Itakuwa kichekesho ukanywa chai bila mkate ama ukala mkate bila kunywa chai!

    Ili MUUNGANO upatikane ilitakiwa MAPINDUZI yafanyike kwanza kama tunavyoona ktk Historia Tarehe 12 Januri 1964 MKOLONI WA KIARABU ALIPINDULIWA na ndani ya miezi 3 baadaye Tarehe 26 Aprili, 1964 MUUNGANO ukapatikana.

    MUUNGANO HOYEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  12. Ni muhimu waelewe ya kuwa Tanzania siyo nchi ya kuchezea Kijeshi!

    ReplyDelete
  13. Hiyo MSULI WA MAJESHI ilikuwa ni kama sehemu ya Sherehe tu ktk Maadhimisho ya Miaka 50 ya Muungano, na hivyo SINEMA kamili ni pale watakapo fanya nyoko!

    Ni wazi tuna mapungufu kidogo tu katika mambo machache ya ndani ambayo yana rekebishika yakiwemo, Ufisadi, Rushwa na machache yaliyobaki 3 au ma 4 hivi kama Kero za Muungano, LAKINI UWEZO WA KUILINDA NCHI TUNAO.

    Cha moto watakiona!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...