Timu nzima ya Tanzania Movie Talents kutoka kampuni ya Proin Promotions Limited wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza safari ya kuelekea Mwanza kwaajili ya shindano la kutafuta Vipaji vya Uigizaji Tanzania ambapo shindano hili litaanzia katika Kanda ya Ziwa katika Mkoa wa Mwanza Kuanzia tarehe 5 April 2014 mahali ni Isamilo Lodge.
Mdau Karimu Muhidin Michuzi na Baadhi ya vijana wa kazi katika timu ya kusaka vipaji wakiwa tayari kwa safari ya Mwanza.
Mabasi yakiwa tayari kwa safari ya Mwanza.

Timu nzima ya Kampuni ya Proin Promotions Limited imeondoka leo jijini Dar Es Salaam kuelekea Mkoani Mwanza kwaajili ya kuendesha Shindano la Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania ambapo Kwa kuanza shindano hili litaanzia Mkoani Mwanza Katika Kanda ya Ziwa.

Usaili wa Kutafuta vipaji utafanyika mnamo tarehe 5 mwezi huu katika ukumbi wa Isamilo lodge ambapo vijana wengi wanaomba kuhudhuria kwa wingi ili kuweza kuonyesha vipaji vyao.

Zoezi la kusaka Vipaji katika Kanda ya ziwa utafanyika kwa Siku nne kuanzia tarehe 5 mwezi huu na pia kwa kanda ya Ziwa Usaili utafanyika katika Mikoa Miwili ya Kigoma na Mwanza.

Proin Promotions Limited imeamua kusaka vipaji ili kuweza kuinua tasnia ya filamu nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...