Mabasi yaliyokuwa yamebeba timu nzima ya Proin Promotions Limited yakiwa yamewasili Mkoani Mwanza Usiku huu.
Baadhi ya Timu ya Wafanyakazi Kutoka Kampuni ya Proin Promotions Limited ambao ndio waendeshaji na wasimamiaji wa Mashindano ya Kusaka Vipaji vya uigizaji Tanzania yajulikanayo kama Tanzania Movie Talents wakiwa wanashuka katika Moja ya Basi lililokuwa limebeba wafanyakazi na timu nzima ya Proin Promotions Limited mara baada ya kuwasili mkoani Mwanza Usiku huu.
Timu nzima ya Proin Promotions Limited imewasili salama usiku huu katika Jiji la Mwanza ikitokea Mkoani Dar Es Salaam, tayari kwa kuanza zoezi la Kusaka vipaji vya uigizaji Tanzania, Zoezi hilo limeanzia Kanda ya Ziwa katika Mkoa wa Mwanza ambapo mashindano hayo yataanza tarehe 5 aprili.
Mashindano haya yatafanyika Mkoani Mwanza kwa siku Tatu kuanzia tarehe 5 hadi 9 mshindi wa kwanza atakayepatikana atajinyakulia kitita cha Shilingi laki tano.
Tunaomba Vijana na wakazi wa Jiji la Mwanza na Vitongoji vyake waweze kujitokeza kwaajili ya kuonyesha vipaji vyao ili kuweza kuendelea ujuzi na vipaji vyao vya kuigiza Tanzania na kukuza tasnia ya filamu Nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...