Na Abdulaziz Video, Lindi
Mfuko wa Afya Ya Jamii (CHF)Kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi wamewezesha kupimwa kwa Afya za Madereva Boda boda wa kata ya Kiwalala wilayani Lindi baada ya kufuzu mafunzo ya Udereva.
Mafunzo yaliyotolewa chini ya Mpango shirikishi wa Polisi Jamii Mkoani Humo.
Akiongea na madereva Boda boda mara baada ya kuwatunuku vyeti vya kufuzu mafunzo hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,Kamishna Msaidizi Renatha Mzinga ametoa wito kwa wahitimu hao kujali afya zao kila wakati ambapo aliwahimiza kujiunga na mfuko wa Afya ya jamii ili kupunguza gharama za Tiba kwa Mwaka.
Aidha Kamanda Mzinga aliwataka kutii Sheria za Usalama barabarani na kuacha kuendeshwa na Abiria anaemchukua Kwa Usalama wa maisha yao 'Najua sasa ni madereva makini baada ya kupewa mafunzo haya na leo kuwakabidhi vyeti vyenu ninahakika sasa utoendeshwa na abiria wako fuata sheria kila wakati na ujenge Tabia ya ya urafiki na askari tofauti na ilivyo kwa madereva wengi kuogopa askari kwa kuwa wanavunja sheria kwa makusudi"alimalizia Kamanda Mzinga 
Awali Meneja wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Lindi,Fortunata Kullaya alieleza kuwa kupitia Mpango wa CHF tayari ofisi yake imeanza Utaratibu wa kuyafikia makundi mbalimbali katika Programu ya Kata kwa kata ambapo utoa vipimo Bure kupitia madaktari Bingwa wanaoongozana nao 
"Mfuko wa Chf sasa ndio mkombozi wenu ndugu zangu kwa kuwa unajiunga kwa pesa ndogo na unatibiwa kwa watu 6 wa kaya moja kwa Mwaka tumieni fursa hii muhimu na kama ulivyoona leo tumeamua kuja kuwapima Bure ili nanyi mjue afya zenu nah ii itasaidia kupata Tele kwa tele katika zahanati zenu toka serikali kuu"Alisema Kullaya' 
Jumla ya waendesha Bodaboda 29 waliohitimu mafunzo ya kuendesha bodaboda walikabidhiwa Vyeti na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi na baadae kupata Fursa ya kupimwa magonjwa mbalimbali na kupata Ushauri wa Afya chini ya Mpango wa Kuhamasisha Jamii Kujiunga Na CHF pamoja na Tiba Kwa Kadi Mkoani Lindi
Baadhi ya waendesha Bodaboda wa kata ya Kiwalala wakimsikiliza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi(hayupo Pichani)katika hafla fupi ya kukabidhiwa Vyeti baada ya kuhitimu mafunzo ya Udereva

Mwendesha Bodaboda Bw Daudi Nanjeka Hamis  akipimwa Afya yake  katika kampeni inayoendeshwa na Mfuko wa Afya Ya Jamii(CHF) ya upimaji wa hiari iliyofanyika katika hafla ya kukabidhi vyeti kwa
wahitimu

Meneja wa Nhif/chf mkoa wa Lindi,Bi Fortunata Kullaya akitoa elimu ya kujiunga kwa mfuko wa afya ya jamii kwa waendesha bodaboda waliohitimu,Kushoto ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi na Afisa mtendaji wa kata ya Kiwalala Lindi
Kamanda wa polisi mkoa wa Lindi,Maafisa wa jeshi hilo na Meneja wa Bima ya afya na waendesha bodaboda katika picha ya pamoja
Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi akikabidhi cheti cha kuhitimu mafunzo hayo kwa Mwenyekiti wa waendesha bodaboda Bw Saidi Mchinga katika hafla iliyofanyika katika ofisi ya kata ya Kiwalala wilaya ya Lindi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...