Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa , Dkt Agnes Kijazi amefungua rasmi warsha ya matumizi ya mfumo wa GEOCLIM katika hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam. Warsha hii imeanza rasmi tarehe 8 na itaendelea hadi tarehe 12 Aprili 2014.

GeoCLIM ni mfumo unaosaidia kutoa takwimu za uhakika za taarifa za hali ya hewa kwa kipindi cha miaka mingi (muda mrefu), kwa kuziweka taarifa hizo katika mfumo uliorahisi kutumia (gridded) Dkt Kijazi alisema lengo la warsha hiyo ni kuongeza uelewa wa ukusanyaji wa takwimu za hali ya hewa za muda mrefu kwa kutumia mfumo wa GeoCLIM.

Hivyo kusaidia Mamlaka kutoa takwimu za mabadiliko ya hali ya hewa kwa wakati katika kusaidia sekta mbalimbali kama vile kilimo, ujenzi, nishati, maji, n.k.

Aliongezea kusema mfumo huu unatarajiwa kuongeza uwezo wa Malaka katika uchambuzi wa taarifa za hali ya hewa na hivyo kukabiliana na majanga yatokanayo na mabadiliko ya hali ya hewa (Climate Change) nchini. Mwisho alisema anatarajia washiriki wa warsha hiyo wataweza kuutumia vyema mfumo huo ambao ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi yetu.

Dkt Kijazi aliwashukuru ICPAC na mradi wa PREPARED kwaajili ya kuandaa na kufadhili warsha hiyo ya mafunzo. Kwa watumishi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa.

Imetolewa na Monica Mutoni;Ofisi ya Uhusiano Mamlaka ya Hali ya Hewa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...