Kamanda Ras Makunja wa Ngoma Africa band ni mwanamuziki mpiganaji
aliyepachikwa majina mengi ya utani kutokana na matukio na vibweka vyake.
Unapoutaja muziki wa dansi wa Tanzania maarufu kama "Bongo Dansi" jina la
Mwamuziki Ebrahim Makunja aka Kamanda Ras Makunja na mzimu wake wa "Ngoma Africa band" aka FFU-Ughaibuni ama ukipenda waite "Watoto wa Mbwa"
au Viumbe wa ajabu "Anunnaki Aliens" yenye makao yake kule Ujerumani, vyote hivyo sawa.
Mwanamuziki Kamanda Ras Makunja wa FFU-Ughaibuni, tunamtaja kuwa
Mpiganaji na mmoja wa watunzi wachache sana wa muziki wa dansi ambaye nyimbo au tungo zake zina uzito na ujumbe mkubwa kwa jamii.Maana nyingine
nyimbo zake zina mafunzo fulani
Pamoja na sifa hizo mwanamuziki huyu
Kamanada Ras Makunja na mzimu wake "Ngoma Africa Band" ukimsikiliza sana
utagundua kuwa ujumbe ulio katika nyimbo zake mara nyingine haulezeki rohoni,
kwa jinsi unavyolenga au kuzungumzia kero fulani katika jamii
Kwa tabia hizi
yeye na bendi yake wamejikuta wakiitwa "Watoto wa Mbwa" yaani wasione kitu lazima watabwaka !
Mara nyingine Mtunzi huyu Kamanda Ras Makunja aliyeipindua akili kazi yake,anapoona nyimbo zake zimekuwa cheche za moto huwa anapooza
kwa kupeleka ujumbe mzuri kwa jamii wenye kuziteka nyoyo za wengi
na kuweza kuzipiga meseji roho za walio wengi "Bongo Tambarare"
Hapo kamanda Ras Makunja na kikosi chake cha Ngoma Africa Band wanaonekana kuwa watoto wazuri lakini tabia zao ni kama ngozi hazibadiliki wawapo jukwaani ni sawa na askari wa kutuliza ghasia FFU kwa sababu wanajua
wazi tabia za washabiki wao za kupenda mdundo live wenye kasi kubwa
Kwa mtindo huu wamefanikiwa kuteka mamilioni ya washabiki nje na ndani ya ughaibuni.
Ras Makunja na Muzimu wake "Ngoma Africa Band" wapo ndani ya medani
ya muziki wa dansi takribani miaka 21 na kushika chati katika majukwaa
ya kimataifa.
inasemekana Ngoma Africa band ina himaya yake inayoitwa "Anunnaki Empire"
himaya ya viumbe wa ajabu (wasanii na waliowazunguka) katika makao ya bendi,wakiwemo mafundi mitambo ambao kazi yao ni kuhakikisha kila kitu
kinacho fanywa ni " Extraordinary" mpaka mziki wenyewe ni "Extraordinary Bongo Dansi". Himaya yao haina uwoga bali inatishia wapinzani wao.
Mwanamuziki Ras Makunja inasemekana hatumii ulevi wa aina yoyote hile wa
kuvuta sigara au ganja, bali ni mtu wa mazoezi makali ya kimwili na kihisia,
mazoezi ambayo watu wengi wanadai kuwa yanamsaidia kuongoza kikosi chake
anaposafiri na kufanya tour ndefu, pengine katika nchi zenye utamaduni tofauti na wa afrika.
Kamanda Ras Makunja kufanya nae kazi inabidi uwe mjeshi sio mchezo,kwa sababu hana mdhaa katika kibarua chake.
hivi karibuni inasemekana amesharekodi kibao kipya kinachoitwa " Myonge Mnyongeni ! Haki yake Mpeni" wimbo ambao utatolewa baadaye.
Muziki wa bendi hiyo maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya unasikika pia katika tuvoti at www.ngoma-africa.com pia www.reverbnation.com/ngomaafricaband
Kamanda Ras Makunja wa Ngoma Africa band mwanamuzik i mpiganaji
Kamanda Ras Makunja wa Ngoma Africa band (kulia) na kikosi chake
Kamanda mkuu wa kikosi maalumu ughaibuni,field marshal ras makunja
ReplyDeleteaka mkuu wa himaya ya viume ajabu anunnaki,kiongozi wa watoto wa mbwa,baba unakubalika nyimbo zenu zina mijiwe mizito
mkulu kulu mungwana kamanda ras makunjas mzee wa kufuga mabundi,naona bado unatisha
ReplyDelete