Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizawadiwa meza yenye ramani ya Tanzania na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya rufaa ya Haydom,Dkt.Olav Espegren.  Kinana pia alizungumza na Uongozi sambamba na Watumishi wa hospitali hiyo ya Rufaa ya Haydom wilayani Mbulu,mkoani Manyara.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akimshukuru Diwani wa kata ya EShkesh kupitia chama cha CUF,Ndugu Naftari Kitandu alipohudhuria mkutano wa hadhara wa CCM,katika shule ya sekondari ya Yaeda chini,wilayani Mbulu mkoani Manyara.


Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakaji wa mji wa Mbulu na vitongoji vyake,kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Mbulu,Kinana aliwataka wananchi wa mji huo kuachana na siasa zisizo na tija badala yake wajikite katika miradi mbalimbali ya kujiletea maendeleo na si vinginevy.Katibu Mkuu Ndugu Kinana ameambatana na Katibu wa NEC Itikad,siasa na Uenezi Nape Nnauye,wakiwa mkoani Manyara kwenye ziara ya Kukagua kuhimiza na kusukuma miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Chama,kukagua maandalizi ya uchaguzi ya serikali za mitaa,kusikiliza kero za wananchi na kuzitafututia ufumbuzi.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndug Kinana akiwa amembatana na Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wananchi wa mjini Mbulu walipokuwa wakiwasili kwenye mkutano wa hadhara mkoani Manyara. 
 Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa mbulu wakishangilia jambo kwenye mkutano wa hadhara wa CCM,uliofanyika mjini Mbulu mkoani Manyara.
 Sehemu ya umati wa wakazi wa mji wa mbulu wakishangilia jambo kwenye mkutano wa hadhara wa CCM,wakati  Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye alipokuwa akihutubia mjini Mbulu mkoani Manyara.
 Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye akihutubia umati wa watu katika viwanja vya Mbulu mjini,wilayani Mbulu mkoani Manyara.



Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisaidia kuweka zege kweye renta,ikiwa ni sehemu ya ushiriki wa ujenzi wa jengo la nyumba ya Mwalimu shule ya sekondari ya Yaeda chini Wilayni Mbulu mkoani Manyara.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana (anaendesha mashine ya kushindilia) akishiriki ujenzi na ukaguzi wa daraja la Haydom wilayani Mbulu mkoani Manyara.
Nape Nnauye akishiriki ujenzi wa daraja la Haydom wilayani Mbulu mkoani Manyara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 29, 2014

    Huyu Nape anaweza kuja kuwa Rais! Je anaigiza au anafanya kweli?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...